• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wizara ya Ujenzi Yapongezwa

imewekwa Tar: November 3rd, 2021

RC RUKWA AIPONGEZA SERIKALI KWA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA

 

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa, Mheshimiwa Joseph Mkirikiti ameipongeza Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kwa kuendelea kuboresha miundombinu ya barabara nchini.

Ameyasema hayo wakati akifungua semina ya mafunzo kwa wadau wa usafirishaji kuhusu Sheria ya Udhibiti Uzito wa Magari ya Afrika Mashariki ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2018 inayofanyika kwa siku moja mkoani humo.

 

Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa, miundombinu ya barabara mkoani Rukwa imepitia changamoto mbali mbali, awali kutoka Tunduma hadi Sumbawanga ilikuwa ikichukua masaa nane hadi siku nzima hali kadhalika kutoka Sumbawanga kuelekea mikoa ya Tabora na Mwanza wananchi walikuwa wakipata mateso makubwa sana na ndio maana Serikali kupitia awamu tofauti imekuwa ikiweka msisitizo wa maboresho ya miundombinu kwa barabara zote nchini.

“Mkoa wa Rukwa unafunguka pande zote iwe kutoka Sumbawanga kwenda Tunduma, lakini pia kutoka Sumbawanga kwenda Tabora na Kigoma, hivyo tunalolijadili hapa ni suala pia la maendeleo ya mkoa wetu, iwapo miundombinu hii itatumika vizuri maana yake mkoa huu unaweza kuwa ni pito la bidhaa zinazotoka Congo DRC, hivyo kujipanga kimkakati katika utunzaji wa miundombinu ya barabara kunalenga kupandisha pato la mkoa wetu, lakini pia pato la Taifa.

“Mambo yote tunayo yajadili hapa yanahusu matumizi ya rasilimali za nchi hasa fedha kwa ajili ya maendeleo yetu, hivyo tunapojadili utekelezaji wa sheria hii ni lazima tutilie maanani dhana nzima ya uzalendo, kwani sheria inaweza kuwepo lakini kama hatutakuwa wazalendo katika kusimamia utekelezaji wake basi hatutakuwa tumefanya jambo jema”, amesema Mkirikiti.

Awali, akimkaribisha Mgeni Rasmi, Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa, Denis Bandisa, amewapongeza waandaaji wa mafunzo hayo kwa kuuchagua mkoa wa Rukwa kuwa mwenyeji wa semina ya mafunzo kwa wadau wa usafirishaji kuhusu Sheria ya Udhibiti uzito wa Magari na kuongeza kuwa jukwa hilo ni fursa moja wapo kwa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa kukutana na wadau wa mkoa huo na kubadilishana mawazo.

Kwa upande wake Kaimu Meneja wa TANROADS mkoa wa Rukwa Mhandisi Mgeni Mwanga, amesema kuwa mafunzo hayo ni muendelezo wa utoaji elimu ya Sheria ya Udhibiti Uzito wa Magari ya Afrika Mashariki ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2018 ambayo yamekuwa yakitolewa kwa wadau wa usafiri wa barabara nchini tangu mwaka 2018 kabla ya kuanza kutumika rasmi kwa sheria hiyo mwezi Machi mwaka 2019.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wadau wa usafirishaji mkoani Rukwa, wameipongeza Serikali kwa kuandaa mafunzo hayo kutokana na ukweli kwamba wengi wao hawana uelewa wa kutosha juu ya sheria hiyo ya Udhibiti Uzito wa Magari ya Afrika Mashariki, na hivyo wamekuwa wakifanya makosa mengi kwa kukosa uelewa.

Semina ya mafunzo kwa wadau wa usafirishaji kuhusu Sheria ya Udhibiti Uzito wa Magari ya Afrika Mashariki ya mwaka 2016 na kanuni zake za mwaka 2018 inayofanyika mkoani Rukwa imeandaliwa na Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, kupitia Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), na inahusisha wadau kutoka mikoa ya Rukwa na Katavi.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa