• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Ziara ya Kamati ya Siasa CCM Mkoa

imewekwa Tar: March 11th, 2022

CCM YARIDHISHWA MRADI WA MAJI NAMANYERE KUKAMILIKA

Na. OMM Rukwa

Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Rukwa kimeridhishwa na hatua ya serikali kufanikiwa kukamilisha mradi wa maji katika mji wa Namanyele wilaya ya Nkasi ambapo umegharimu shilingi Bilioni 1.3 hadi sasa na utanufaisha wananchi 27,000.

Kauli hiyo imetolewa jana (10.03.2022) na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Rukwa Rainer Lukala wakati alipoongoza Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya Mkoa huo kukagua miradi ya maendeleo ikiwa ni utekelezaji wa Ilani.

“Tumeridhishwa na jinsi Suwasa ilivyofanikiwa kukamilisha mradi huu ambao utakuwa suluhisho la kero ya maji katika mji wa Namanyere ambapo tumeelezwa kuwa umefikia asilimia 98 .Sasa tuitake serikali kufikisha umeme kwenye eneo hili la chanzo ili maji yaanze kusukumwa kwenda majumbani” alisema Lukala.

Mwenyekiti huyo wa CCM aliongeza kusema changamoto ya miradi ya maji kutokamilika kwa kipindi kilichopangwa lazima sasa ifike mwisho kwa kuwa serikali ya Chama cha Mapinduzi imekuwa ikitoa fedha kwa wakati.

“Changamoto ya umeme haipaswi kuendelea, Mkuu wa Mkoa (Joseph Mkirikiti) fuatilia Tanesco ili miradi ya maji iweze kuanza kazi mapema na kero ya wananchi kukosa maji safi na salama iishe” aliagiza Lukala.

Akitoa taarifa ya mradi huo, Mkurugenzi Mtendaji wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Sumbawanga (SUWASA) Mhandisi Gibon Nzowa alisema jumla ya shilingi 1,398,289,294/- kati ya shilingi 1,775,096,000/- zimetumika kukamilisha mradi huo wa maji ambao utaongeza uzalishaji maji toka lita 600,000 kwa siku hadi lita 1,800,000 kwa siku.

Mhandisi Nzowa alibainisha kuwa mradi huo umefanikiwa kusambaza bomba kuu lenye urefu wa kilometa 3.9 na umesambaza mabomba ya maji yenye urefu wa kilometa 6.5 katika mji wa Namanyere.

Mhandisi Nzowa aliwaeleza wajumbe hao kuwa kazi inayosubiriwa kwa sasa ni TANESCO kufikisha umeme katika mtambo wa kusukuma maji ili wananchi waanze kupata huduma.

Katika hatua nyingine Kamati hiyo ya Siasa ya CCM mkoa ilikagua pia mradi wa maji kijiji cha Katongolo wilaya ya Nkasi ambao unatekelezwa na Wakala wa Maji Safi na Usafi wa Mazingira (RUWASA) na tayari umegharimu shilingi 202,518,074/- kati ya shilingi 349,732,107/- na umefikia asilimia 80.

Meneja wa Ruwasa Nkasi Mhandisi Shafii Shabani alisema mradi huo utanufaisha wananchi 2,734 wa kijiji cha Katongolo huku akitaja changamoto ya umeme kukwamisha zoezi la majaribio ya kusambaza maji kwenye vituo vya kuchotea (BP) 14 zilizojengwa.

Akijibu hoja za tatizo la umeme kukwamisha miradi hiyo kuanza kazi, Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Mkirikiti ameahidi kulifuatilia na kuchukua hatua za haraka ili Tanesco wafikishe huduma hiyo.

Pamoja na miradi ya maji, Kamati ya Siasa ya Halmashauri Kuu ya CCM Mkoa wa Rukwa imekagua pia mradi wa ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya kata ya Paramawe itakayogharimu shilingi Milioni 470 ambayo ujenzi wake utakamilika Juni mwaka huu.

Kamati hiyo ya Siasa imemaliza ziara wilaya ya Nkasi na wiki ijayo itaendelea na ziara ya ukaguzi wa miradi katika wilaya ya Kalambo.

Mwisho.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa