Serikali kupitia Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule ambaye pia alikuwa kaimu Mkuu wa Mkoa wa Rukwa alikwenda kuzitembelea kaya 336 zilizoathiriwa na mvua na upepo mkali uliotokea usiku wa tarehe 8.12.2018 na kuahidi kutoa kilo 5 za unga wa sembe kwa kila kaya kama kianzio huku misaaada mingine ikiendelea kusubiriwa
Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga mkoani Rukwa imeibuka mshindi wa kitaifa wa mbio za za Mwenge wa Uhuru uliowashwa mwezi April katika viwanja vya magogo Mkoani Geita na na kuzimwa mwezi oktoba siku ya kumbukumbu ya kifo cha Mwl. Julius Nyerere katika Kiwanja Mkwakwani Mkoani Tanga na kukimbizwa katika Halmashauri 195 nchini.
“Watanzania wanalipa kodi zao, fedha ni nyingi sana, tunazipeleka kwenye miundombinu na kule ambako hakuna tunasikia hapa, kwamba jamani tunahitaji barabara Fulani TARURA barabara Fulani TANROAD lakini udhibiti wa barabara unakuwa sifuri, hiuli jambo nisingependa liendelee na iwe agenda tupate taarifa na tuambiwe namna walivyodhibiti, sio kusema tu kwamba tutafanyia kazi, tusikie wapi barabara imeharibiwa na halmashauri imedhibiti namna gani,”Alisistiza.
Katika mwaka wa fedha 2018/2019 shilingi bilioni 13.8 zimeidhinishwa kwaajili ya matengenezo ya barabara na madaraja na bilioni 2.7 kwaaajili ya miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Rukwa.
Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa