• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Baada ya maafa RC Wangabo aunga mkono juhudi za wananchi kukarabati shule

imewekwa Tar: December 28th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amechangia shilingi milioni tatu ili kuharakisha ukarabati wa ujenzi wa shule ya msingi Msia pamoja na shule ya sekondari Kipeta zote za bonde la ziwa rukwa, Wilayani Sumbawanga ikiwa ni kuunga mkono juhudi za wananchi katika kurudisha miundombinu ya shule hizo zilizoharibika baada ya upepo na mvua kali iliyonyehs amwanzoni mwa mwezi huu.

Kati ya fedha hizo shilingi milioni mbili zitatumika katika shule ya msingi Msia na shilingi milioni moja zitatumika kuikarabati shule ya sekondari kipeta ambapo zimebaki wiki mbili shule hizo kufunguliwa na wanafunzi kutakiwa kuendelea na masomo.

Mh. Wangabo aliwashukuru wananchi waliojitokeza kuchangisha fedha kwaajili ya ukarabati wa shule ya msingi Msia zilizofikia kiasi cha shilingi 5,595,000/= ambapo wananchi wa kawaida walichangia shilingi 5000/=, wafanyabiashara wadogo shilingi 20000/=, mfangabiashara wa kati shilingi 50000/= na wafugaji shilingi 100000/= ambapo fedha hizo zinatarajiwa kufanya ukarabati na ujenzi wa madarasa manane.

Awali akisoma taarifa ya harambee ya ukarabati wa shule Mtendaji wa kijiji cha Msia Andrew Sanga alieleza mikakati ya kijiji kuwa ni kuongeza vyumba vya madarasa vitatu, na ofisi moja ya walimu na msingi umeshaaza kujengwa, kukusanya michango kwa wananchi ambao bado kuchangia na hivyo kutimiza lengo la kujenga madarasa nane, ofisi mbili ndani kabla ya shule kufunguliwa mwanzoni mwa mwezi wa kwanza.

“Mheshimiwa mkuu wa mkoa mapungufu yaliyopo ni kama ifuatavyo, bati, madirisha, nondo, misumari, madirisha, milango na rangi, ili kukamilisha majengo tunayoendelea kuyajenga kwani shule hiyo yenye wanafunzi 866 ina uhitaji wa madarasa 22,” Alibainisha.

Katika kuunga Mkono juhudi hizo Mh. Wangabo alisema,”Pamoja na pongezi ambazo nilizitoa kwa wadau wote ambao wamechangia, na mimi nipende kushirikiana nanyi, nitachangia vifaa ambavyo inaweza ikawa mabati, au inaweza ikawa saruji, kulingana na hesabu zitakazokuwa zinapigwa na Mkurugenzi pale, nitachangia hivyo vifaa kwa shilingi milioni mbili.”

Pia aliwasihi mafundi wa madarasa hayo kujiahidi kuzingatia ubora katika ujenzi kuliko ilivyokuwa imejengwa hapo awali na kuwaomba wachukulie kazi hiyo ni kama ya kujitolea mchango wao katika kuunga juhudi za wananchi kumaliza shule hiyo.

Pia kwa upande wa shule ya sekondari ya Kipeta alichangia shilingi milioni moja kama mwanzo wa harambee itakayofanyika mwanzoni mwa mwezi wa kwanza mwaka 2019 ili kuhamasisha wananchi wa kijiji cha kipeta kuweza kuiboresha shule hiyo ambayo iliezuliwa mapaa yote pamoja na baadhi ya nyumba 4 za walimu ikiwemo ya mwalimu Mkuu.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi wa halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga Sebastina Mwilima alisema kuwa tayari halmashauri imeshaagiza vifaa vyenya thamani ya shilingi milioni 23 kwaajili ya kufanikisha zoezi la kukarabati shule hizo ambapo shule ya msingi Msia madarasa manne yalianguka na shule ya sekondari Kipeta, madarasa, mabweni pamoja na nyumba za waalimu kuezuliwa mapaa.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa