• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Ufugaji

Mifugo

SEKTA YA MIFUGO

Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa Mifugo 

Zoezi la utambuzi wa mifugo kwa njia ya hereni za kieletroniki ‘Electronic Ear tags’ kutekeleza Sheria ya Utambuzi, Usajili na Ufuatiliaji wa Wanyama Na.19 ya mwaka 2008 lilianza mwezi Agosti, 2021 na linafanyika katika Halmashauri zote. Hadi kufikia tarehe 31 Desemba, 2022 zoezi lilipositishwa na Serikali jumla ya ngombe 264,190 mbuzi 1,570; kondoo 457 na punda 605 walikuwa wametambuliwa.

Usimamizi wa utekelezaji wa Sheria katika Utoaji wa Huduma za Mifugo

Mwaka 2022/2023 Baraza la Veterinari Tanzania (Veterinari Council of Tanzania - VCT) kwa kushirikiana na Mkoa na Halmashauri lilifanya ukaguzi wa kawaida (Routine Inspection) katika Halmashauri. Shughuli zilizofanyika ni pamoja na usajili na ukaguzi wa wataalamu wa afya ya Wanyama na miundombinu ya Vituo vya utoaji wa huduma za afya ya Wanyama na kukagua maeneo yanayojihusisha na uuzaji wa dawa na vifaa tiba vya wanyama. Jumla ya Vituo/maduka 28 yalikaguliwa ndani mkoa na hatua kuchukuliwa kwa wale waliokutwa na makosa

Vilevile, Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (Tanzania Medicines and Medical Devices Authority - TMDA) Ofisi ya Kanda – Mbeya kwa kushirikiana na Wataalamu wa Mifugo wa Manispaa ya Sumbawanga ilifanya ukaguzi wa utekelezaji wa sheria miongoni mwa Wadau katika maeneo yanayojihusisha na uuzaji wa dawa na vifaa tiba vya wanyama.

Ukaguzi wa miundombinu ya zao na Wadau waliokatika mnyororo wa thamani wa zao la nyama

Mwaka 2023 Bodi ya Nyama Tanzania (Tanzania Meat Board - TMB) Ofisi ya Kanda – Mbeya kwa kushirikiana na Wataalamu wa Mifugo Mkoa na Halmashauri ilifanya ukaguzi wa utekelezaji wa sheria miongoni mwa Wadau katika mnyororo wa thamani wa nyama na miundombinu yao katika Halmashauri ikiwa ni pamoja na hali ya usajili na viwango vya ubora wa machinjio, Minada Awali ya mifugo, wafanyabiashara wa mifugo na nyama. Miundombinu iliyokaguliwa ni minada 4, machinjio 3, magari ya kubebea nyama 4 na maduka ya nyama 54 ili kuhakikisha nyama inayozalishwa iko katika ubora na salama kwa afya ya walaji.

Ufuatiliaji Matukio ya Magonjwa ‘Field Surveillance’

Katika ufuatiliaji wa magonjwa ya wanyama, Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) ziliwasilisha jumla ya Taarifa 2,337 (Animal Diseases Surveillance Field Report) ziliwasilishwa ZVC Sumbawanga. Tathmini ya uwasilishaji taarifa za matukio ya kila wiki inaonesha kati ya Kata 97 zilizopo, jumla ya Kata zilizowasilisha (completeness) ni 74, sawa na asilimia 76 kimkoa na uwasilishaji wa Halmashauri kwa wakati muafaka (timeliness) ni asilimia 80 kimkoa.. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inaendelea kuzihimiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kufuatilia na kuwasilisha taarifa za matukio ya magonjwa kwa wakati muafaka.

Kinga na Udhibiti dhidi ya Magonjwa mbalimbali ya mifugo

Chanjo zilizosambazwa na TVLA kwa Halmashauri/Maduka ya Dawa

Kituo cha Kanda cha TVLA Sumbawanga kiliuza na kusambaza chanjo ndani ya Mkoa kupitia wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Halmashauri, Watoa huduma wa sekta binafsi (Maduka ya Dawa za Mifugo) na mashamba ya mifugo. Kwa mujibu wa Taarifa za TVLA, chanjo zilizouzwa na kusambazwa mwaka 2022/2023 ni:-

Aina na Dozi za Chanjo zilizouzwa na kusambazwa na TVLA

Na.
Aina ya Chanjo
Jumla ya Dozi
 
S19 Brucella
25
 
Chambavu - BQ
900
 
Chambavu na Kimeta (Blanthrax)
2,600
 
Homa ya Mapafu ya Mbuzi -CCPP
3,500
 
Homa ya Mapafu ya Ng’ombe - CBPP
6,100
 
Kimeta - Anthrax
20,000

Mdondo -Newcastle (I - 2)
 1,641,040

Jumla 
1,674,165








Chanzo: Taarifa za kila mwezi za TVLA Sumbawanga 2022/2023 

Uogeshaji mifugo kudhibiti Magonjwa yanayoenezwa na Kupe

Udhibiti wadudu ambukizi na sumbufu ulifanyika katika maeneo mbalimbali kwa njia ya kuogesha mifugo. Katika kipindi cha mwaka 2021/2022 na mwaka 2022/2023 Mkoa ulipokea dawa za kuogesha mifugo jumla ya lita 2,067.5 aina ROL - DIP 330EC® - Alphacypermethrin 30g/l, Chlorpyrifos 300g/l zenye thamani ya shilingi milioni 92.97 kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kuzigawa katika Halmashauri.

Pamoja na jitihada hizo za Serikali kiwango cha kuogesha mifugo kwa kutumia majosho bado kipo chini katika Halmashauri zote. Hii ni inachangiwa na matumizi yasiyoendelevu ya majosho hususan kipindi cha msimu wa kilimo kutokana na kukosekana kwa njia za mifugo kuelekea katika majosho, baadhi ya wafugaji kutokuwa tayari kuogesha mifugo yao katika majosho yaliyopo, usimamizi hafifu pamoja na kukosekana kwa majosho katika baadhi ya maeneo ya ufugaji yenye ng’ombe wengi (mtawanyiko wa majosho) hususan Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Aidha, upatikanaji wa taarifa za matumizi ya pampu za mikono upo chini ukilinganisha na hali halisi.

Katika mwaka 2022/2023 majosho 39 yalifanyakazi na kuwezesha michovyo 1,735,112 (ng’ombe 1,452,998; mbuzi 155,006; kondoo 124,373; mbwa 2,521 na punda 214). 

Pia kulikuwa na minyunyizo 3,750,000 kwa kutumia pampu za mikono (ng’ombe 3,081,405; mbuzi 341,670; kondoo 247,259; nguruwe 70,218; mbwa 9,064 na punda 384). Jedwali Na. 30. Dawa (Viuatilifu) zilizotumika katika kuogesha mifugo maeneo mbalimbali ni Alphacypermethrin & Chlorpyrifos, Alphacypermethrin, Amitraz 12.5% na Cypermethrin. 

 

 

Maeneo yaliotengwa kwa ajili ya malisho

Maeneo ya malisho yapo katika Halmashauri za Kalambo, Nkasi na Sumbawanga ambazo ziliandaa na kuyawasilisha katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hapa chini

Maeneo ya malisho Mkoa wa Rukwa

Halmashauri
Kijiji
Ukubwa wa Eneo
Jina la kikundi
Kalambo
Matai Asilia
Ekari 5
Livestock and Fishfarm
Mbuluma
Ekari 5
Uviwakimnu
Nkasi
Chalatila
Ekari 5
Wafugaji
Paramawe B
Ekari 5
Chapakazi group
Sumbawanga DC
Kalambanzite
Ekari 5
Uviwakika
Miangalua
Ekari 5
Umoja wa Vijana Makozi

 

Mifugo ni Mingi na Ngozi ni nyingi Mkoa wa Rukwa , Ngozi iliyokaushwa kwa njia ya Chumvi

Ngozi iliyokaushwa kwa hewa


Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo (kulia) alipotembelea kiwanda cha nyama cha SAAFI ambacho ni kiwanda pekee kilichopo Mkoa wa Rukwa. 

Ombi kwa Wawekezaji

Pamoja na kuwepo kwa ng'ombe wengi kufikia nusu ya idadi ya wananchi wanaoishi Mkoa wa Rukwa bila ya kuiongelea mifugo mingine tunaona kuwa kuna uhitaji mkubwa wa uwepo wa viwanda vingi vya kusindika nyama pamoja na malighafi zinazotokana na mifugo hiyo ikiwemo ngozi, pembe, n.k.


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa