• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kilimo

Uwekezaji katika kilimo

Wakulima wengi katika Mkoa huu ni wadogo wadogo wanaolima kati ya hekta 0.5 – 2.0 na wakulima wa kati wanaoliama kati ya hekta 2.0 – 4.0. Hivi karibuni tumeanza kupata wakulima wakubwa wanaolima hekta 300 – 1,000. Kwa sasa tunao wakulima/mashamba matatu (3) ya MSIPAZI, EMPIEN na MAJINJA ambao wanalima kilimo cha kibiashara cha mashamba makubwa. Uongozi wa Mkoa tunaendelea kushirikiana nao kwa kuweka mazingira wezeshi ili wazalishe kwa tija na kuanzisha viwanda vya kusindika mazao wanayozalisha pia kuwa waelimishaji na soko kwa wakulima wanaowazunguka.

  •  Changamoto za Kilimo katika Mkoa.

Changamoto kubwa zinazokwamisha kukua kwa sekta ya kilimo katika Mkoa wa Rukwa ni pamoja na:-

Matumizi kidogo ya pembejeo  za Kilimo (mbolea, Mbegu na Viuatilifu)

Matumizi  madogo ya  zana  za kisasa za  Kilimo  katika kulima, kuvuna na kuandaa mazao kabla hayapekwa katika soko. 

Upungufu wa maafisa ugani kwa ajili ya kutoa elimu na stadi za Kilimo ili kuongeza uzalishaji.

   Matumizi madogo ya fursa kubwa ya umwagiliaji iliyopo katika mkoa.

Teknolojia za kisasa kutoka katika vituo vya utafiti kutowafikia wakulima kwa wakati.

Ukosefu wa vitendeakazi kwa Maafisa Ugani katika ngazi zote.

Mikakati ya kuendeleza sekta ya kilimo.

Mkoa umeweka mikakati ambayo inateelezwa ili kukabiliana na changamoto zinazokwamisha ukuaji wa sekta ya kilimo. Mikakati hiyo ni kama ifuatavyo;

Kutumia vituo vya raslimali za kilimo katika kutoa elimu ya kilimo.

Mkoa wa Rukwa una jumla ya Vituo vya rasilimali za Kilimo 9 (Kalambo DC 1, Nkasi DC 5, Sumbawanga DC 2 na Sumbawanga MC 1). Vituo sita (6) vilivyowekewa vifaa vinatumika kwa ajili ya kutoa mafunzo kwa wakulima, kupata machapisho rejea, kupata teknolojia za Kilimo kwa wakulima waliopo katika Kata.

Upatikanaji wa masoko ya  mazao ya kilimo.

Soko kubwa na la uhakika la mahindi  kwa wakulima wa Mkoa wetu ni kupita Wakala wa Chakula wa Taifa (NFRA)ambao hununua kwa bei ambayo hukidhi gharama za uzalishaji wa Mahindi . Kwa kuzingatia ukweli kuwa Serikali siyo soko pekee la mazao yetu inatulazimu tushirikiane na sekta binafsi, mfano TCCIA na wadau wengine kutafuta masoko ya mazao yetu ndani na nje ya nchi na kuwa tayari kushindana na wazalishaji wengine wa mahindi kwa kuongeza ubora na kupunguza gharama za uzalishaji. Aidha, katika msimu huu tumedhamiria kuwakumbusha watendaji wa Halmashauri kuvisimamia vyama vya Ushirika vilivyopo na kusimamia uanzishwaji wa vyama vipya vya ushirika wa mazao (AMCOS) .

Kuongeza matumizi ya zana za kisasa za kilimo.

Mkoa kwa kutambua kwamba tuna zana za kilimo (trekta) chache, tunaendelea na juhudi za makusudi za kuwezesha wakulima kupata zana bora za kilimo. Tulianza kuwaunganisha wakulima na shirika la SUMAJKT na sasa tutaendelea kuwaunganisha wakulima na NDC na Agricom ili waweze kukopa matrekta .  Mkoa utaendelea kuhakikisha kuwa zana zilizopo katika mkoa zinatumika ipasavyo katika kuongeza tija katika kilimo.

Kuboresha kilimo cha umwagiliaji

Mkoa utaendelea kutoa elimu juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji katika skimu za umwagiliaji zilizopo na kuwachukulia sheria baada ya kuwaelimisha kwa wale watakaobainika kuhushika na uharibifu wa mazingira. Tutaendelea kufanya kaguzi wa hali ya miundombinu ya umwagiliaji kabla na baada ya msimu wa mvua ili kubaini uharibifu uliopo katika miundombinu ya umwagiliaji pamoja na kutoa elimu kwa umoja wa umwagiliaji juu ya umuhimu wa kuchangia katika kukarabati miundombinu ya umwagiliaji. Mkoa unaendelea kuwahamasisha wakulima kujiunga pamoja na kujenga baadhi ya miundombinu ya umwagiliaji kwa kutumia guvu zao.

Matumizi madogo ya pembejeo.

Mkoa unaendelea kushirikiana na TFRA kuhakikisha kuwa Mbolea inapatikana katika Mkoa kupitia mfumo unaojulikana kama ‘Bulk Procurement System’

Mfumo huu unasimamiwa na sheria ya usimamizi wa mbolea namba 9 ya mwaka 2009, kifungu cha 51 na kanuni za Mwaka 2017. Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (Tanzania Fertilizer Regulatory Authority-TFRA) wamepewa kazi ya kusimamia upatikana na usimamizi wa sheria ya mbolea katika Nchi.

Aidha Mkoa unaendelea kushirikiana na Mamlaka ya udhibiti wa ubora wa mbegu Tanzania (TOSCI) katika kuhakikisha kuwa mbegu zinazo wafikia wakulima ni zile zenye ubora. Tunaendelea kusisitiza kuwa wakulima wajiunge pamoja na kuangiza mbolea na mbegu moja kwa moja kwa wazalishaji ili kuondokana na uchakachuaji na kupunguza gharama.

Upungufu wa Maafisa Ugani.

Serikali inaendelea kuajiri watumishi ikiwemo wale wa kilimo ili kukidhi mahitaji ya maafisa hao. Vile vile tumepokea maagizo ya Mhe. Waziri Mkuu ya kupunguza watumishi waliopo makao makuu ya Halmashauri na kuwapangia maeneo ya kata na vijiji ambako kuna mahitaji makubwa ya watumishi hao.  Vile vile Mkoa unashirikiana na sekta binafsi katika kutoa huduma za ugani kwa wakulima waliopo katika Halmashauri zetu.

Matumizi ya zana za kilimo.

Matumizi ya zana za kilimo zinazokokotwa na wanyamakazi (Maksai) Mkoa ni asilimia 74, matumizi ya matrekta ni asilimia 4 na matumizi ya jembe la mkono ni asilimia 22.  Mkoa una jumla ya matrekta makubwa yapatayo 121, madogo 114, combine harvester 11 na maksai 105,855 kama inavyonekana katika jedwali hapo chini.

  • Halmashauri
  • Idadi ya  maksai
  • Idadi ya matrekta makubwa
  • Idadi ya matrekta madogo
  • Idadi ya mashine za kuvumia
Sumbawanga (M)
  • 7,953
  • 36
  • 19
  • 2
Sumbawanga (W)
  • 20,982
  • 22
  • 39
  • 2
Nkasi
  • 33,124
  • 42
  • 31
  • 5
Kalambo
  • 43,796
  • 21
  • 15
  • 1
Jumla 
  • 105,855
  • 121
  •  104
  • 11


Mahindi ni miongoni mwa Zao Kubwa linalolimwa kwa wingi Mkoa wa Rukwa 

Kilimo cha Alizeti nacho kinapewa kipaumbele katika mkoa wa Rukwa 

Maboga nayo yamekuwa ni biashara kubwa katika Mkoa wa Rukwa 

Ngano ni miongoni mwa mazao yanayoshamiri na kulimwa kwa wingi Mkoani Rukwa 




Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa