• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Huduma za Mifugo

SEKTA YA MIFUGO

HUDUMA ZA AFYA YA MIFUGO

Ukaguzi wa Vituo vya Huduma (Maduka ya Dawa) za Mifugo

Wakaguzi kutoka Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (Tanzania Medicines and Medical Devices Authority - TMDA) walifanya ukaguzi Maalum katika maduka yanayouza dawa za mifugo katika Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na Mji wa Namanyere katika Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi tarehe 15 na 16 Oktoba, 2019. Aidha, Mkaguzi kutoka Ofisi ya Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania (VCT), Dodoma alifika na kufanya ukaguzi wa kawaida katika baadhi ya maeneo kuanzia tarehe 17.10.2019 hadi 20.10.2019 kwa kushirikiana na Daktari wa Mifugo - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Wataalamu wa Mifugo wa Halmashauri husika (Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga, Halmashauri za Wilaya ya Kalambo na Nkasi).

Mkaguzi wa Nyanda za Juu Kusini - Ofisi ya Msajili wa Baraza la Veterinari Tanzania (VCT), Dodoma alifika na kufanya ukaguzi wa kawaida katika baadhi ya maeneo kuanzia tarehe 17.2.2020 hadi 20.2.2020 kwa kushirikiana na Wataalamu wa Mifugo wa Halmashauri husika (Halmashauri ya Manispaa Sumbawanga, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi na Kalambo).

Matokeo ya Kaguzi hizo, Jumla ya maeneo 26 yalikaguliwa ambapo, Dawa aina ya VETOXY 20®,  BIOSOL® , ALBENDEX®, LEVAZOLE® , OXYZASH Bolus®  na EWP Topical Application  ambazo hazikuwa na usajili wa TMDA na dawa aina ya PEN & STREP® ya kampuni ya Norbrook na PEN-STREP 20/25® ya kampuni ya Farvet zilizokutwa hazijahifadhiwa katika jokofu (nyuzi joto 2O C – 8O C) ziliondolewa katika soko (madukani), wamiliki 9 walitozwa faini jumla Sh. 4,700,000/= kwa mujibu wa Sheria na Kanuni za Veterinari zinazosimamiwa na VCT, wawili walilipa ada Sh. 280,000/=,  wawili (10) walionywa waache biashara ya kuuza dawa za mifugo kwa hiari yao hadi hapo watakapokamilisha taratibu za usajili wa maduka/vituo vyao katika Baraza la Veterinari - VCT na maduka matano (5) yalifungwa yalifungwa na VCT kutokana na kukiukwa Sheria, Kanuni na Taratibu za uendeshaji wa Maduka ya Dawa za Mifugo. Aidha, Mkaguzi alipopita mwezi Februari, 2020 Ukaguzi haukufanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga baada ya Mkurugenzi wa Halmashauri kuomba zoezi hilo liahirishwe kwa muda wa mwezi mmoja katika eneo lake ili aweze kuongea na wamiliki wa maduka yaliyopo.

Ufuatiliaji wa uhamishaji holela wa mifugo na migogoro ya ardhi

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na ZVC Sumbawanga na wadau wengine (Ofisi ya Mkuu wa Wilaya Nkasi, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi na Meneja wa Pori la Akiba Lwafi) ilifanya ufuatiliaji wa ng’ombe 702 waliokuwa wameingizwa katika Pori la Akiba la Lwafi kinyume na Sheria na kufanikiwa kusuluhisha mgogoro huo. Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na wahusika kulipa faini ya shilingi 13,960,000 kwa ng’ombe 698 waliokuwa wamebaki baada ya ndama 4 kufa.

Ufuatiliaji wa Mayai yanayoingizwa kutoka nje ya Mkoa bila Vibali

Serikali  ilifanikiwa kukamata Wadau kumi na nne (14) na mayai 56,220 (trei 1,874)  yaliyoingizwa bila Vibali na kuwatoza faini wadau hao jumla ya shilingi 3,380,000/= aidha, kati ya trei hizo zilizokamatwa jumla ya mayai 10,920 (trei 364) yanayosadikiwa kuingizwa kutoka Zambia kupitia Tunduma yaliteketezwa.

Pamoja na hatua hizo, Wadau walipewa elimu ya kuzingatia Sheria na Kanuni katika usafirishaji wa mayai.

Ufuatiliaji Matukio ya Magonjwa ‘Field Surveillance’

Katika ufuatiliaji wa magonjwa ya wanyama, Mamlaka za Serikali za Mitaa (MSM) ziliwasilisha jumla ya Taarifa 845 (Animal Diseases Surveillance Field Report) ziliwasilishwa ZVC Sumbawanga, ambapo katika utaratibu wa kila wiki taarifa 799 na utaratibu wa EMAi taarifa 46. Kiwango cha uwasilishaji taarifa za kila wiki kutoka ngazi ya Vijiji/Kata kipo chini sana. Ofisi ya Mkuu wa Mkoa inaendelea kuzihimiza Mamlaka za Serikali za Mitaa kufuatilia na kuwasilisha taarifa za matukio ya magonjwa kwa wakati muafaka.

Kinga na Udhibiti dhidi ya Magonjwa mbalimbali ya mifugo

Chanjo zilizosambazwa na TVLA kwa Halmashauri/Maduka ya Dawa

Kituo cha Kanda cha TVLA Sumbawanga kiliuza na kusambaza chanjo ndani ya Mkoa kupitia wadau mbalimbali ikiwa ni pamoja na Halmashauri, Watoa huduma wa sekta binafsi (Maduka ya Dawa za Mifugo) na mashamba ya mifugo. Kwa mujibu wa Taarifa za TVLA, chanjo zilizouzwa na kusambazwa mwaka 2019/2020 ni:-

  Aina na Dozi za Chanjo zilizouzwa na kusambazwa na TVLA

Na.
Aina ya Chanjo

Jumla ya Dozi


Mdondo -Newcastle (I - 2)

                              1,878,500        


Homa ya Mapafu ya Ng’ombe - CBPP

5,000


Chambavu na Kimeta (Blanthrax)

2,850


Chambavu

3,750


S19 Brucella

250


Jumla 

1,890,350

Chanzo: Taarifa za kila mwezi  za TVLA Sumbawanga  2019/2020  

Uogeshaji mifugo kudhibiti Magonjwa yanayoenezwa na Kupe

Udhibiti wadudu ambukizi na sumbufu ulifanyika katika maeneo mbalimbali kwa njia ya kuogesha mifugo. Katika kipindi cha mwaka 2019/2020, mkoa ulipokea viuatilifu vya kuogesha mifugo jumla ya lita 617 aina ya TikTik Amitraz 12.5% na lita 188 aina ya Paranex ‘Alphacypermethrin’ kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi na kuzigawa katika Halmashauri.

Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kwa kushirikiana na Wizara ya Mifugo na Uvuvi ilifanya hamasa na ufuatiliaji wa utekelezaji kampeni ya kukarabati au kujenga majosho na kuogesha mifugo. Ambapo katika kipindi cha mwaka 2019/2020 majosho yaliyokarabatiwa ni 12 (majosho 8 kwa ufadhili wa Wizara na 4 kwa fedha za Halmashauri) na josho 1 limejengwa na wafugaji binafsi. Hivyo kumekuwa na ongezeko la majosho mazima kutoka 53 hadi 61 na majosho yaliyofanyakazi kutoka 40 hadi 56 mwaka 2019/2020 ukilinganisha na mwaka 2018/2019.

Pamoja na jitihada hizo za Serikali kiwango cha kuogesha mifugo kwa kutumia majosho bado kipo chini katika Halmashauri zote. Hii ni inachangiwa na  matumizi yasiyoendelevu ya majosho hususan kipindi cha msimu wa kilimo kutokana na kukosekana kwa njia za mifugo kuelekea  katika majosho, baadhi ya wafugaji kutokuwa tayari kuogesha mifugo yao katika majosho yaliyopo,  usimamizi hafifu pamoja na kukosekana kwa majosho katika baadhi ya maeneo ya ufugaji yenye ng’ombe wengi (mtawanyiko wa majosho) hususan Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga. Aidha, upatikanaji wa taarifa za matumizi ya pampu za mikono upo chini ukilinganisha na hali halisi.

Katika mwaka 2019/2020 majosho 56 yalifanyakazi na kuwezesha michovyo 1,804,507 (1,512,599 ya ng’ombe; 238,877 ya mbuzi; 51,567 ya kondoo na 1,879 ya mbwa). Jedwali Na. 30 na 32.

Pia kulikuwa na minyunyizo 1,228,365 kwa kutumia pampu za mikono (946,864 ya ng’ombe; 180,609 ya mbuzi; 61,725 ya kondoo; 32,144 ya nguruwe na 7,023 ya mbwa) Jedwali Na. 30. Dawa (Viuatilifu) zilizotumika katika kuogesha mifugo maeneo mbalimbali ni Amitraz 12.5%, Alphacypermethrin na Cypermethrin. 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa