• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Historia

Mkoa wa Rukwa ulianzishwa mwaka 1974 kwa kumega sehemu ya Mkoa wa Tabora (Mpanda) na Mbeya (Sumbawanga).  Mnamo mwezi Julai 2010 Serikali ya Awamu ya Nne iliridhia kugawanywa kwa Mkoa wa Rukwa na kuanzishwa kwa Mkoa mpya wa Katavi.

Jiografia ya Mkoa

Mkoa wa Rukwa upo kati ya Latitudo 70 – 90 Kusini ya Ikweta na Longitudo 30 – 320 Mashariki ya Grinwichi. Mkoa huu unapakana na Mikoa ya Katavi upande wa Kaskazini na Songwe upande wa Kusini Mashariki; Aidha, unapakana na nchi za Zambia upande wa Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo upande wa Magharibi. Eneo la juu sana katika Mkoa wa Rukwa linapatikana Malonje katika Nyanda za juu za Ufipa ambalo ni Mita 2,461 Juu ya Usawa wa Bahari na eneo la chini zaidi ni Ziwa Tanganyika lenye Mita 773 Juu ya Usawa wa Bahari.

 Eneo la Mkoa

Mkoa huu una eneo la kilomita za mraba 27,765,  kati ya hizo Kilomita za mraba 22,844 (82.3%) ni za nchi kavu na Kilomita za mraba 4,921 (17.7%) ni za maji kama ilivyoainishwa katika Jedwali 

Eneo Mkoa wa Rukwa mwaka 2017

Wilaya
Halmashauri ya Wilaya/ Manispaa
Eneo Km. za mraba
Eneo la Ardhi. 
Eneo la Maji. 
Km2
%
Km2
%
S’wanga
S’wanga MC
1,329
1,329
100.0
0
0
S’wanga DC
8,871
8,203
92.5
668
7.5
Nkasi
Nkasi
13,124
9,375
71.4
3,749
28.6
Kalambo
Kalambo
4,441
3,937
88.7
504
11.3
Jumla
 
27,765
22,844
82.3
4,921
17.7

 

Muundo wa Mkoa Kiutawala 

Mkoa wa Rukwa umegawanyika katika Wilaya tatu (3), zenye Halmashauri nne (4), Tarafa 16, Kata 97, Vijiji 339 Vitongoji 1,825 Kaya 185,076 na Mitaa 167. Wilaya hizo ni Sumbawanga, Kalambo na Nkasi. Mkoa unajumuisha Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga, Nkasi na Kalambo. Aidha, ndani ya Mkoa kuna Mamlaka za Miji Midogo miwili ambazo ni Namanyere Wilaya ya Nkasi na Laela Wilaya ya Sumbawanga. Yapo majimbo matano (5) ya Uchaguzi ambayo ni: Sumbawanga Mjini na Kwela – Wilaya ya Sumbawanga; Kalambo – Wilaya ya Kalambo; Nkasi Kusini na Nkasi Kaskazini – Wilaya ya Nkasi.

 Eneo la Muundo wa Utawala Mkoa wa Rukwa 2017

Wilaya
Halmashauri 
Eneo Km. Za mraba
IDADI YA
Tarafa
Kata
Vijiji
Vitongoji
Mitaa
Majimbo ya Uchaguzi
S’wanga
S’wanga MC
1,329
2
19
24
173
167
1
S’wanga DC
8,871
4
27
114
494
0
1
Nkasi
Nkasi
13,124
5
28
90
721
0
2
Kalambo
Kalambo
4,441
5
23
111
439
0
1
Jumla
 
27,765
16
97
339
1825
167
5

 

Idadi ya Watu 

Kwa mujibu wa Sensa ya watu na Makazi ya Mwaka 2012, Mkoa wa Rukwa ulikuwa na Wakazi wapatao 1,004,539 ambapo Wanawake ni 517,228 na Wanaume ni 487,311. Mkoa pia unazo Kaya 185,076 na wastani wa wakazi kwa Kaya moja ni watano (5).  Ongezeko hili ni sawa na wastani wa asilimia 3.2% kwa Mwaka.

Mwaka 2017 Mkoa unakisiwa kuwa na  Wakazi wapatao 1,192,373 ambapo Wanawake wanakisiwa kuwa 613,942 na Wanaume 578,431 Mchanganuo wa takwimu za idadi ya watu na makazi kwa mwaka 2012 na maoteo ya mwaka 2017 ni kama ilivyo katika jedwali 

 Idadi ya Wakazi Kiwilaya kwa Mwaka 2012
HALMASHAURI
IDADI
WAKAZI KWA KAYA
ME
KE
JUMLA
KAYA
WASTANI
Sumbawanga MC

100,734

109,059

209,793

41,644

4.8

Sumbawanga DC

149,062

156,784

305,846

52,084

5.0

Nkasi DC

137,041

144,159

281,200

50,597

5.3

Kalambo DC

100,474

107,226

207,700

40,751

4.9

Jumla

487,311

517,228

1,004,539

185,076

5.0

 

 

 Maoteo ya Idadi ya Wakazi Kiwilaya kwa Mwaka 2017
HALMASHAURI
IDADI
WAKAZI KWA KAYA
ME
KE
JUMLA
KAYA

WASTANI

Sumbawanga MC

119,570

129,451

249,021

51,879

4.8

Sumbawanga DC

176,934

186,100

363,035

72,607

5.0

Nkasi DC

162,666

171,115

333,780

62,977

5.3

Kalambo DC

119,261

127,276

246,537

50,313

4.9

Jumla

578,431

613,942

1,192,373

237,776

5.0

 

 







Hali ya hewa

Mkoa wa Rukwa una hali ya hewa ya Kitropiki ambapo wastani wa joto ni Sentigredi 13 katika baadhi ya maeneo kwa miezi ya Juni na Julai hadi Sentigredi 27 kwa miezi yenye joto jingi ya Oktoba na Desemba. Mkoa umebahatika kuwa na mvua za kuaminika kwa miaka mingi; mvua za Mkoa huu ni wastani wa milimita 850 kwa mwaka zikinyesha kuanzia mwezi wa Novemba – Mei. Kiangazi huanza mwezi Juni mara baada ya majira ya mvua hadi mwezi wa Oktoba.

Shughuli za Kiuchumi  

Kiuchumi, wakazi wa Mkoa wa Rukwa wanajishughulisha na, Kilimo cha mazao ya chakula na biashara, ufugaji, sekta ya utalii, madini, uvuvi, viwanda  vidogo pamoja na biashara ndogondogo. Shughuli kuu ya Kiuchumi ni Kilimo, ambapo mazao ya chakula yanayolimwa kwa wingi ni Mahindi, Mpunga, Viazi vitamu, Viazi mviringo, Mihogo, Maharage na Ulezi.  Mazao ya biashara yanayolimwa kwa wingi ni Alizeti, Ngano, Ufuta na Michikichi. Aidha, ziada ya Mazao ya chakula kama Mahindi, Mpunga, Maharage, Ulezi, Ngano, Shayiri na Karanga hutumika pia kama mazao ya biashara. Ufugaji unabaki kuwa shughuli kuu muhimu ya pili ya uchumi katika Mkoa wa Rukwa. Mifugo inayofugwa kwa wingi  ni Ng’ombe, Mbuzi, Nguruwe, Kondoo, Punda na Kuku.

Pato la Mkoa wa Rukwa

Pato la Mkoa limekuwa likiongezeka mwaka hadi mwaka, kutoka kiwango shilingi 2,718,398 (milioni) sawa na asilimia 3.41 mwaka 2014 hadi kufikia shilingi 3,180,865 (milioni) sawa na asilimia 3.50 mwaka 2015. Kuhusu pato la mwananchi kwa mwaka, nalo pia limekuwa likiongezeka kutoka shilingi 1,618,883 mwaka 2014, hadi kufika Shilingi 1,840,724 mwaka 2015. Hii ni kwa mujibu wa takwimu za mwisho zilizotolewa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) mwaka huu 2016.

Historia ya Viongozi kwa Mkoa wa Rukwa

 Orodha ya Wakuu wa Mkoa tangu mkoa ulipoanzishwa. 

Na
Jina Kamili 
Tarehe aliyoanza 
Tarehe Aliyoondoka 
1.
Mr. M.G. Baruti
1, Januari 1974
21, Februari 1983
 2.
Mr. E.S. Mnyawami
22, Februari 1983
5, Juni 1984
3.
Mej. Gen. T. Kiwelu
6, Juni 1984
14, Novemba 1988
4.
Capt. P.N. Kafanabo
15, Novemba 1988
9, Disemba 1990
5.
Dr. K.M. Kiwanuka
10, Disemba 1990
8, Septemba 1991
6.
Mr. A.S. Aljabri
9, Septemba 1991
5, Novemba 1993
7.
Mr. C.M. Mzindakaya
6, Novemba 19993
30, Disemba 1995
8.
Mej. S. Nswima
31, Disemba 1995
10, Disemba 1997
9.
Capt. Jaka M. Mwambi
11, Disemba 1997
7, Februari 2003
10.
Capt. G.H. Mkuchika
8, Februari 2003
20, Agosti 2005
11.
Daniel Ole Njoolay
6, Februari 2006
15, Septemba 2011
12.
Eng. Stella Martin Manyanya
16, Septemba 2011
30, Agosti 2015
13.
Magalula Said Magalula
31, Agosti 2015
13, Machi 2016
14.
Zelote Stephen Zelote
13, Machi 2016
26, Oktoba 2017
15.
Joachim leonard Wangabo
26, Oktoba 2017


Orodha ya Makatibu Tawala wa Mkoa tangu kuanzishwa kwa Mkoa

 

Namba
Jina
Tangu
Mpaka
1.
J. Matiko
1.1.1974
29.3.1975
2.
D.F.P Ringo
30.3.1975
18.8.1976
3.
R.S. Lukindo
19.8.1976
6.1.1980
4.
S.K. Masinde
7.1.1980
2.1.1984
5.
C.T. Kisanji
2.1.1984
17.11.1985
6.
T.N. Machume
18.11.1985
16.2.1989
7.
A.A.K. Mwasajone
17.2.1989
17.2.1994
8.
P.A. M Chikira
20.5.1995
14.2.1997
9.
W. Ngirwa
15.2.1997
15.11.1998
10.
H.N.M. Kachechele
16.11.1998
3.4.2006
11.
Innocent Mwenda
4.4.2006
7.7.2009
12.
Salum .M.Chima
25.1.2010
18.1.2014
13.
Smythies E. Pangisa
18.1.2014
29.2.2016
14.
Tixon Tuyangine Nzunda
9.9.2016
23.5.2017
15.
Bernard Mtandi Makali
23.5.2017


Matangazo

  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Mwongozo wa Mfumo wa Anwani za Makazi April 20, 2022
  • Hotuba ya Bajeti ya WN -OR TAMISEMI 2022/23 April 20, 2022
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • JAMII ISHIRIKIANE NA WALIMU KUKUZA TAALUMA

    February 16, 2023
  • Kampeni Upandaji Miti

    February 07, 2023
  • TASAF

    February 05, 2023
  • RAS Mchatta akagua miradi

    January 26, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0739862632

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa