• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Huduma za Afya

SEKTA YA AFYA, LISHE NA USTAWI WA JAMII

HALI YA WATUMISHI WA SEKTA YA AFYA KATIKA MKOA

Mkoa una jumla ya watumishi 1980 kati ya watumishi 4,523 wanaohitajika hivyo kufanya upungufu wa watumishi 2537 kama ilivyo katika Jedwali Na.1. hapa chini:-

Jedwali Na.1 .Mchanganuo wa watumishi wa Afya 

Mamlaka

Mahitaji

Waliopo

Upungufu/ Ziada
HM Sumbawanga

698

370

328(47%)

HW Sumbawanga

1207

429

778(64%)

HW Nkasi

920

433

487(53%)

HW Kalambo

1232

428

804(65%)

Hospitali ya Rufaa ya Mkoa

466

320

146(31%)

Jumla (Mkoa)

4523

1980

2543(56%)

 

 

Jedwali Na.2.Vituo vya kutolea huduma za afya kwa ujumla

Ngazi ya Kituo 

Umiliki

Jumla 
RRH
Halmashauri
Binafsi 
FBO
Taasisi za Serikali
Taasisi nyingine
Hospitali

1

4

0

2

0

0

7

Kituo cha Afya

0

16

1

8

0

0

25

Zahanati

0

188

15

9

7

0

219

Kliniki Maalum

0

0

0

0

0

0

0

Jumla (Mkoa)

1

240

18

20

6

0

251

 

2.0 Taarifa Ya Hali  Miradi Ya Miundombinu Ya Kutolea Huduma Za Afya Katika Mkoa.

 2.1. Ujenzi wa Hospitali za Halmashauri.

 

Ujenzi wa Hospitali za Halmashauri unaendelea katika Halmashauri nne ndani ya Mkoa. Halmashauri zinazotekeleza ujenzi wa Hospitali ni Halmashauri za Wilaya za Nkasi, Kalambo, Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga na Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ambapo hadi kufikia Juni, 2023 jumla ya Shilingi 12,897,500.00 zilikuwa zimepokelewa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hizo ambapo kiasi cha Shilingi 12,700,000,000 zikitoka Serikali Kuu na Kiasi cha shilingi 301,000,000.00 kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri, kama inavyoonekana kwenye jedwali Na3

 

 

 

Jedwali Na.3 .Mapokezi ya Fedha za ujenzi wa Hospitali za Halmashauri

Na
Halmashauri

Fedha iliyotolewa (Serikali Kuu)

Fedha iliyotolewa (Mapato ya Ndani)

Jumla ya fedha iliyotolewa

1
Sumbawanga MC

2,550,000,000

11,500,000.00

2,561,500,000

2
Sumbawanga DC

3,400,000,000

0

3,400,000,000

3
Nkasi  DC

3,400,000,000

146,000,000

3,546,000,000

4
Kalambo DC

3,350,000,000

40,000,000

3,390,000,000


Jumla

12,700,000,000

301,000,000

12,897,500,000

2.2 Ujenzi wa vituo vya Afya.

Hadi kufikia Septemba, 2023 Mkoa umetekeleza ujenzi wa vituo vya afya 21 ambavyo vimepokea jumla ya shilingi 9,703,374,500 Kati ya fedha hizo shilingi 528,374,000 ni fedha za mapato ya ndani, shilingi 8,900,000,000 ni fedha kutoka Serikali kuu, kama inavyoonekana kwenye jedwali hapa chini.

Jedwali Na. 4. Fedha zilizopokelewa kwa ajili ya ujenzi na upanuzi wa vituo vya Afya

Na
Halmashauri

Fedha iliyotolewa (Serikali Kuu)

Fedha iliyotolewa (Mapato ya Ndani)

Jumla ya fedha iliyotolewa

1
Sumbawanga MC

1,800,000,000

76,374,500

1,876,374,500

2
Sumbawanga DC

1,400,000,000

580,000,000

1,980,000,000

3
Nkasi  DC

3,300,000,000

47,000,000

3,347,000,000

4
Kalambo DC

2,400,000,000

100,000,000

2,500,000,000


Jumla

8,900,000,000

803,374,500

9,703,374,500

Mkoa umejenga jumla ya vituo vya Afya 21 kupitia fedha zilizokelewa kati ya hivyo vituo 7vimenza kutoa huduma za upasuaji wa dharura, 17 vinatoa huduma kwa wagonjwa wan je na Vituo vya Afya 4 bado haviajaanza kutoa huduma. Hii imesaidia kuboresha huduma pamoja na kupunguza vifo vya akina mama na Watoto wachanga vitokanavyo na uzazi

2.3. Ukamilishaji wa maboma ya Zahanati.

            

Kwa kipindi cha kuishia Septemba, 2023 Mkoa umepokea jumla ya shilingi 1,597,537,465 kwa ajili ya umaliziaji wa maboma 31 ya Zahanati kwenye halmashauri zote nne za Mkoa wa Rukwa, Kati ya fedha hizo, shilingi 1,522,537,465 ni fedha za Serikali kuu na shilingi 75,000,000 ni fedha za Mapato ya ndani. Mchanganuo wa fedha za ukamilishaji wa maboma ya zahanati umeonyeshwa kwenye Jedwali Na.5

Jedwali Na.5.Ujenzi wa Maboma katika Halmashauri

Na
Halmashauri

Fedha iliyotolewa (Serikali Kuu)

Fedha iliyotolewa (Mapato ya Ndani)

Jumla ya fedha iliyotolewa

1
Sumbawanga MC

250,000,000

25,000,000

275,000,000

2
Sumbawanga DC

304,209,079

0

304,209,079

3
Nkasi  DC

664,219,307

50,000,000

714,219,307

4
Kalambo DC

304,109,079

0

304,109,079


Jumla

1,522,537,465

75,000,000

1,597,537,465

2.4. Utekelezaji wa Programu ya huduma endelevu za maji na usafi wa mazingira vijijini (Sustainable Rural Water Supply and Sanitation Program “SRWSSP”

Hadi sasa Mkoa umepokea jumla ya shilingi 2,432,293,134 kwa ajili ya utekelezaji wa programu ya huduma endelevu za maji na usafi wa mazingira vijijini (The Sustainable Rural Water Supply and Sanitation Program-SRWSS). Fedha hizo zimepokelewa kwa awamu tatu kati ya 2019/2020, 2020/2021 na 2022/2023. Fedha hizo ni kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu ya maji na usafi kwenye vituo vya kutolea huduma za afya, shughuli za uratibu wa program ngazi ya Mkoa na Halmashauri na uhamasishaji wa usafi wa mazingira kwenye jamii. Hadi sasa jumla ya vituo 61 vya kutolea huduma za afya vimepatiwa fedha za ujenzi wa miundombinu ya Maji na usafi wa mazingira ndani ya Mkoa. Mchanganuo wa fedha zilizopokelewa umeonyeshwa kwenye jedwali Na.6

Jedwali Na.6.Fedha za utekelezaji wa Mradi wa Usambazaji wa maji na usafi wa mazingira kwenye Vituo vya kutolea huduma za Afya

Halmashauri

Fedha za Awali (2019/2020)

Mavuno ya m waka wa kwanza

Mavuno ya mwaka wa pili

JUMLA

(2020/2021)

(2021/2022)

Kalambo DC

272,830,000

365,920,000

276,462,586

915,212,586

Nkasi  DC

272,830,000

218,080,000

456,140,548

947,050,548

Sumbawanga DC

272,830,000

287,200,000

10,000,000

570,030,000

Jumla

818,490,000

871,200,000

742,603,134

2,432,293,134

2.5. Ujenzi wa Nyumba za Watumishi   

 

Mkoa pia ulipokea jumla ya shilingi. 270,000,000 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba tatu za watumishi (three in one) kwenye Halmashauri tatu za Nkasi, Kalambo na Sumbawanga kupitia mpango wa maendeleo ya ustawi wa Taifa na mapambano dhidi ya UVIKO-19.

2.6. Mapokezi ya Fedha za Miradi kwa Mwaka 2023/2024

Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2023/2024 Mkoa umepokea kiasi cha fedha shilingi  bilioni 3,820,000,000.00  kwa ajili ya ujenzi, ukarabati na ununuzi wa vifaa tiba kwa ajili ya vituo vya kutolea huduma kupitia vyanzo vifuatavyo;- kama inavyoonekana kwenye jedwali hapa chini.

Jedwali Na.7. Mapokezi ya Fedha za Miradi kwa Mwaka wa fedha 2023

 

FEDHA ZA MIRADI ZILIZOPOKELEWA HALMASHAURI KWA MWAKA 2023/2024 

 JUMLA 

 VOTE NAME 

 UJENZI WA HOSPITALI ZA WILAYA 

 ORODHA YA VITUO VYA AFYA  318 VINAVYOJENGWA VINAVYOHITAJI VIFAA 

 UJENZI/UKAMILISHAJI WA VITUO VYA AFYA 

 UKAMILISHAJI WA ZAHANATI  

 ORODHA YA ZANAHATI 564 ZINAZOHITAJI VIFAA 

RukwaRegion







Sumbawanga MC

1,070,000,000

300,000,000

500,000,000

50,000,000

100,000,000

2,020,000,000

Sumbawanga DC

-

-

-

100,000,000

-

100,000,000

Nkasi DC

-

600,000,000

-

200,000,000

100,000,000

900,000,000

Kalambo DC

-

300,000,000

-

400,000,000

100,000,000

800,000,000


1,070,000,000

1,200,000,000

500,000,000

750,000,000

300,000,000

3,820,000,000

kiasi cha fedha shilingi bilioni 3,820,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na ukamilishaji wa maboma ya Zahanati kwa mchanganuo ufuatao;-

Halmashauri ya Manispaa ya Sumbawanga imepokea kiasi cha fedha Jumla ya shilingi bilioni 2,020,000,000/= ambapo kiasi cha shilingi bilioni 1,070,000,000.00 kwa kuendeleza ujenzi Hospitali ya Manispaa Sumbawanga, milioni 500,000,000.00 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya Kata ya Senga na Sumbawanga na  kiasi cha fedha shilingi milioni 50,000,000.00 umaliziaji wa ujenzi wa Zahanati ya Milanzi. Lakini pia Kiasi cha shilingi milioni 400,000,000 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba katika Zahanati Mpya na Vituo vya Afya.

Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi imepokea kiasi cha fedha shilingi milioni 900,000,000.00, ambapo kiasi cha fedha shilingi milioni milioni 700,000,000.00 ni kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na shilingi milioni milioni 200,000,000.00 kwa ajili ukamilishaji wa maboma ya Zahanati 4. Mchakato wa manunuzi unaendelea.

 Halmashauri ya Wilaya Sumbawanga imepokea kiasi cha fedha kiasi cha shilingi 100,000,000 kwa ajili ya ukamilishaji wa Zahanati 2.

Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo kiasi cha fedha shilingi milioni 800,000,000, ampapo shilingi milioni 400,000,000.00 kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi wa Zahanati 8 na kiasi cha fedha shilingi milioni 400,000,000 kwa ajili ya vifaa tiba ngazi ya Vituo vya Afya na Zahanati.

  • Program ya kudhibiti na kupambana na VVU/UKIMWI kupitia Mdau HJMFRI Mkoa umepokea kiasi cha fedha shilingi 160,187,951.00 kwa ajili ya ukarabati wa vituo vya kutolea huduma 10 ambapo kazi ya ujenzi inaendelea.
  • Program ya Usafi wa Mazingira WASH. Mkoa unatarajia kupokea kiasi cha fedha shilingi 2,212,662,000.00 kupitia mpango huu.

 

3.0  HALI YA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA 

 

 3.1. Huduma za kupambana na maambukizi ya VVU na UKIMWI

 

3.2.1. Hali ya Maambuki ya VVU katika Mkoa

Kutokana na ripoti ya utafiti wa kitaifa wa mwaka 2016/2017 “Tanzania HIV Impact Survey” (THIS-2016/2017), kiwango cha maambukizi ya VVU (UKIMWI) Kitaifa kimeshuka kutoka 5.1% had 4.7%, kiwango cha kuwabaini watu wanaokadiriwa kuishi na VVU nchini ni 52.2%, kiwango cha kuwaanzishia dawa za kufubaza makali ya VVU watu waliotambuliwa kuwa na VVU ni 90.9%, na kupungua kwa kiwango cha VVU kwenye damu (Viral Suppression) ni 87.7%. Matokeo ya utafiti huu pia yameonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ya UKIMWI kwa Mikoa ya Nyanda za juu kusini ni wastani wa 4.7% sawa na wastani wa kitaifa na kiwango cha maabukizi kwa Mkoa wa Rukwa ni 4.4% ambacho kimepungua kutoka 6.2% (2011/2012)

3.2.2. Utekelezaji wa Mikakati ya Kitaifa na Kimataifa katika Mapambano dhidi ya Janga la VVU/UKIMWI. 

Kupitia malengo na mikakati ya Kitaifa na Kimataifa ambayo ndiyo dira kuelekea mafanikio katika vita hii. Miongoni mwa Mikakati hiyo ni pamoja na;- Mkakati wa Dunia wa kutokomeza janga la UKIMWI kupitia shirika la Umoja wa Mataifa la kupambana na UKIMWI (United Nations against AIDS-UNAIDS) unaolenga kufikia 95-95-95 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2025 na Mpango wa Taifa wa kufikia sifuri 3 ifikapo mwaka 2030

 

Malengo ya tisini na tano tatu (95, 95, 95) ifikapo Disemba, 2025: Hadi kufikia Septemba, 2023 Mkoa umefanikiwa kutekeleza malengo haya kama ifuatavyo;-

  • Kati ya watu 35,194 wanaokadiriwa kuwa na maambukizi ya VVU/UKIMWI, watu 32,084 tayari wamepima na kutambulika kuwa na maambukizi ambayo ni sawa na 96% kulinganisha na kiwango cha Taifa 95%.
  • Kati ya watu 32,084 waliopima na kutambulika kuwa na maambukizi ya VVU/UKIMWI, watu 31,506 tayari wameunganishwa kwenye huduma za dawa ambayo ni sawa na 99% ulinganisha na kiwango cha Taifa cha 95%.
  • Kiwango cha kufubaa kwa virusi vya UKIMWI mwilini (Viral Suppression level) kwa wateja wanaotumia dawa za kufubaza makali ya virusi vya UKIMWI kimefikia 97% sawa na wateja 29,189 ulinganisha na kiwango cha Taifa 95%.
  • Kiwango cha wateja ambao wamebakia kwenye huduma za dawa kimefikia 99.6%

3.2.3.HUDUMA ZA KINGA DHIDI YA MAAMBUKIZI YA UKIMWI

Mkoa kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo unasimamia miongozo ya utekelezaji wa shughuli mbali mbali za kinga dhidi ya maambukizi ya VVU/UKIMWI kama ifuatavyo:-                    

Huduma za unasihi na upimaji wa VVU                                 

Tohara ya hiari ya Kitabibu kwa wanaume (VMMC).             

Matumizi ya Kondomu                                                               

Huduma za kuzuia maambukizi kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto (PMTCT)

Huduma za uzazi wa mpango                                                  

Huduma za kifua kikuu na UKIMWI (TB/HIV)                        

Huduma za Tiba na Matunzo (CTC)                                        

Huduma ya uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya kikazi (CECAP) 

3.2.4. Mafanikio kwenye eneo la Huduma za Kupambana na VVU/UKIMWI

Kupitia ufadhili wa shirika la HJFMRI katika utekelezaji wa afua za kupambana na UKIMWI, Mkoa umepata mafanikio yafuatayo; -

  1. Kupungua kwa kiwango cha maambukizi ya VVU kutoka 6.2% (2011/2012) hadi 4.4% (2016/2017)
  2. Kufikia malengo ya tisini na tano ya pili kwa asimilia 99.6%.
  3. Idadi ya vituo vya kutolea huduma za tiba na malezi kwa watu wanaoishi na Virusi vya UKIMWI (CTC) imeongezeka kutoka vituo 31 mwaka 2015 hadi vituo 110 kufikia Septemba, 2023.
  4. Idadi ya vituo vya kutolea huduma za ushauri nasihi na upimaji wa VVU imeongezeka kutoka vituo 193 mwaka 2015 hadi vituo 204 kufikia Septemba 2023.

3.2.5.Changamoto katika eneo la huduma za Kupambana na VVU/UKIMWI

Pamoja na mafanikio yaliyopatikana, zipo changamoto mbalimbali ambazo zimekuwa zikijitokeza katika kutekeleza shughuli za kupambana na VVU/UKIMWI kama ifuatavyo; -.

  1. Ukachavu wa magari kwa ajili ya usimamizi elekezi wa huduma za mapambano dhidi ya UKIMWI ngazi ya Mkoa na Halmashauri. Ukiachilia uchakavu wa magari yaliyopo, Mkoa bado unakabiliwa na upungufu wa magari na vyombo vingine vya usafiri kwa ajili ya usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za kupambana na VVU/UKIMWI

3.2.6. Mikakati Ya Mkoa dhidi ya Janga la VVU/UKIMWI

Katika kipindi cha kuandaa mikakati ya Mkoa, tunapaswa kutambua uwepo wa malengo na Mikakati ya Kitaifa na Kimataifa ambayo ndiyo dira kuelekea mafanikio katika vita hii. Miongoni mwa Mikakati hiyo ni pamoja na;-

  • Mpango wa Taifa wa kufikia sifuri 3 ifikapo mwaka 2025 (Sifuri ya kwanza-Hakuna maambukizi mapya, Sifuri ya pili-Hakuna vifo vitokanavyo na UKIMWI, Sifuri ya Tatu-Hakuna unyanyapaa) uliozinduliwa mwaka 2015,
  • Mkakati wa Dunia wa kutokomeza janga la UKIMWI unaolenga kufikia 95-95-95 ifikapo mwishoni mwa mwaka 2030 (Fast-Track-Targets to End Epidemic). Mkakati huu unafuatia mkakati wa awali uliolenga kufikia 90-90-90 ifikapo Disemba, 2020.

Pamoja na mikakati hiyo, Mkoa umejiwekea mikakati ifuatayo katika kupambana na janga la UKIMWI.

Kubaini wahisiwa wa virusi vya UKIMWI hasa wanaume na mabinti ambao hawajapata huduma za upimaji.

Kurudisha watoto kwenye huduma za dawa kwa 98% (98% Retention rate).

Kuongeza kiwango cha kufubaaa kwa virusi kwa Watoto kwa kuhakikisha kuwa Watoto wanapata dawa sahihi za kufubaza virusi vya UKIMWI. (Pediatric formulations)

Kutoa dawa kinga kwa makundi maalumu wakiwemo wanawake wanaonyonyesha (PrEP & PEP).

Kuongeza utoaji wa dawa za ARV kwa utaratibu wa kipindi cha zaidi ya mwezi mmoja (Multi Month Scripting-MMS) ambapo kwa sasa tumeruhusiwa kutoa dawa za miezi sita (6).

Upimaji wa VVU kwa watu wa karibu na mteja aliyetambulika kuwa na maambukizi ya VVU na kusajiliwa kwenye mfumo wa tiba na malezi (Index Case Testing)

Kuhakikisha wateja wote waliosajiliwa kwenye huduma za tiba na malezi wanabakia kwenye huduma hizo (Retention)

Kuhakikisha wateja wote waliosajiliwa kwenye huduma za tiba na malezi wanaostahili kupewa dawa kinga ya Kifua Kikuu, wanapatiwa dawa hizo (TPT)

Kuongeza vituo vya huduma ya tohara (static sites) kwa kila Halmashauri kwa 10% kila mwaka.

3.3. HALI YA HUDUMA ZA KIFUA KIKUU NA UKOMA

3.3.1. HALI YA KIFUA KIKUU KATIKA MKOA 

Mkoa umepiga hatua kadhaa katika kuboresha huduma za Kifua Kikuu na huduma nyingine za afya kwa ujumla kupitia jitihada zinazofanywa na serikali ikishirikiana na wadau mbalimbali hususani shirika la THPS Uhuru (Tanzania Health Promotion support) na AMREF Afya Shirikishi.  Mwaka 2022  wagonjwa 1182  wa Kifua Kikuu waligundulika ikilinganishwa na wagonjwa 1092 mwaka 2021  ikiwa ni ongezeko la asilimia 8.2. Wagonjwa (new and Relapse) 1028 kati ya wagonjwa 1092 wa Kifua Kikuu waliogundulika mwaka 2021 walitibiwa na kupona kwa asilimia 95.1 ikiwa ni zaidi ya lengo la Taifa la uponaji la asilimia 90.

3.3.2. HALI YA UGONJWA WA UKOMA MKOA 

Mkoa umepiga hatua katika kupambana na Ugonjwa wa Ukoma kutoka  wagonjwa 173 wa mwaka 2015  hadi wagonjwa 41 mwaka 2022.Hata hivyo Wilaya ya Nkasi bado haijafikia Kiwango cha kutokomeza Ugonjwa wa Ukoma ambapo ina kiwango cha maambukizi cha 1.2(prevalence rate).

Ili kuweza kutokomeza ukoma mikakati mbalimbali inaendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na kutoa elimu juu ya Ukoma, kufanya kampeni za kutokomeza Ukoma katika maeneo ambayo yana wagonjwa wengi (Hot spot area) hususani mwambao wa Ziwa Tanganyika wilaya ya Nkasi na kuhakikisha dawa mseto za Ukoma (Leprosy-MDT) zinapatikana muda wote, ili kuzuia na kutibu ulemavu utokanao na Ukoma. 

3.3.3. Mafanikio katika kupambana na Kifua Kikuu na Ukoma

  1. Jumla ya wagonjwa 1182 wa Kifua Kikuu wameibuliwa mwaka 2022 ikilinganishwa wagonjwa 1092 mwaka 2021
  2. Wagonjwa wa Kikuu Kifuu wapatao 1028 kati ya wagonjwa 1092 wa Mwaka 2021 walitibiwa na kupona Kifua Kikuu ikiwa ni sawa na asilimia 94.1% ya lengo la Kitaifa la Kitaifa la 90%
  3. Uibuaji wa Kifua Kikuu kwa watoto chini ya miaka kumi na tano ilikuwa 222 /1178= 19% ikilinganishwa na lengo la Kitaifa la asilimia 15
  4.  Mchango wa Jamii Katika uibuaji wa wagonjwa wa Kifua Kikuu ilikuwa wagonjwa 402/1180 sawa na 34.07% .Lengo la kitaifa ni 20%
  5. Wagonjwa wote wa Kifua Kikuu walipimwa hali ya maambukizi ya VVU (100%)
  6. Wagonjwa 167 wa Kifua Kikuu (14.8%) waligundulika na maambukizi ya VVU, na wote walianzishiwa dawa za kufubaza makali ya VVU (100%)
  7. Ugonjwa wa Ukoma umeendelea Kupungua kutoka wagonjwa  68 mwaka 2021 hadi wagonjwa 41 mwaka 2022
  8. Mkoa umeshika nafasi ya kwanza Kitaifa kwa Ubora wa Huduma za Kifua Kikuu mwaka 2022 (BEST PERFORMANCE AWARD: 1ST POSITION).

3.3.4. Changamoto katika kupambana na Kifua Kikuu na Ukoma

Pamoja na mafanikio mengi tuliyopata katika sekta ya afya, Mkoa bado unakabiliwa na changamoto mbalimbali katika kutekeleza shughuli za kupambana na ugonjwa wa Kifua Kikuu na Ukoma kama ifuatavyo;-.

  1. Kukosekana kwa Mashine ya Gene Xpert  Kituo cha Afya Laela Halmashauri ya Sumbawanga na Tarafa ya Kala Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi
  2. Wahisiwa wa Kifua Kikuu kushindwa kumudu gharama za X-ray
  3. Wagonjwa wengi wa Kifua Kikuu na Ukoma kuchelewa kwenda kwenye vituo vya Tiba.
  4. Waratibu wa Kifua Kikuu wa Halmashauri za Wilaya  (DTLCs) hawajapata mafunzo ya uratibu na usimamizi wa shughuli za Kupambana na Kifua Kikuu na Ukoma

3.4.0 Mapambano dhidi ya Malaria

Malaria ni moja kati ya magonjwa kumi yanayoongoza kwa kuwa kuwa na wagonjwa wengi wanaopata huduma za matibabu kwa wagonjwa ya nje (OPD) na wagonjwa wanaolazwa katika Mkoa

Kufuatia utafiti wa Malaria uliofanyika kwa wanafunzi wa shule za Msingi Mkoa wa Rukwa kati ya Julai hadi Agosti 2023 inaonyesha kuwa kiwango cha maambukizo ya Malaria kimepungua kutoka 17% kwa mwaka 2019 hadi 12% kwa mwaka 2023.

 Halmashauri zote zimeonyesha kushuka kwa kiwango cha maambukizi ya Malaria isipokuwa Manispaa ya Sumbawanga ambapo imeongezeka kutoka 0.4% kwa mwaka 2019 hadi 1.7% kwa mwaka 2023.

Aidha takwimu za miezi sita ya Januari hadi Juni mwaka 2023 zinaonyesha kuwa kiwango cha maambukizi ya Malaria kimepungua kufikia wagonjwa 33,847 sawa na asilimia 8.6 ya wagonjwa wote waliotibiwa ukilinganisha na wagonjwa 48,191 sawa na asilimia 10 ya wagonjwa wote waliotibiwa kwa kipindi hicho cha mwaka 2022.

3.4.1. Jitihada za kupambana na Malaria

Kwa kuzingatia madhara yatokanayo na ugonjwa wa Malaria, Mkoa umekuwa ukichukua jitihada mbalimbali ikiwa ni pamoja na;

Kugawa vyandarua kwa akina mama wajawazito na watoto wakati wa mahudhurio ya kliniki na makundi maalum (Wazee, Watoto wanaporuhusiwa baada ya kulazwa kutokana na ugonjwa wa Malaria na WAVIU). Aidha katika kipindi cha miezi sita ya Januari hadi Juni 2023 jumla ya vyandarua 34,912 sawa na asilimia 96 vilitolewa kwa akina mama wajawazito na vyandarua 37,666 sawa na asilimia 80 vilitolewa kwa watoto wanapohudhuria kliniki. Pia vyandarua 2791 vilitolewa kwenye makundi maalum.

Kusambaza mabango yenye ujumbe mbalimbali ambao unahamasisha jamii ‘kupima malaria, kwani si kila homa ni malaria, matumizi ya chandarua kujikinga na malaria, matumizi ya dawa kinga dhidi ya malaria kwa akina mama wajawazito na usafi wa mazingira.

Kuhamasisha jamii kuhusu kujikinga dhidi ya malaria kupitia katika Radio zilizopo katika Mkoa ambazo ni pamoja na Voice FM na Ndingala.

Kuendesha vikao vya hamasa kwa viongozi mbalimbali mbali ikiwa ni pamoja na viongozi wa dini, kimila na watu maarufu ili washiriki katika kuelimisha jamii.

Kuhamasisha jamii kuhusu usafi wa mazingira ili kuondoa mazalio na maficho ya mbu.

3.5. Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto.

Mkoa unaendelea na juhudi za kuboresha huduma za Afya ya uzazi na mtoto hususani katika kupunguza vifo vitokanavyo na matatizo ya uzazi. Hali halisi ya huduma na viashiria vya huduma hizi ni kama ifuatavyo;

  1. Kiwango cha akinamama waliojifungulia katika vituo vya huduma kimeongezeka kutoka asilimia 83 mwaka 2016 hadi asilimia 99 Januari - Juni, 2023 ambayo ni zaidi ya kiwango cha kitaifa cha asilimia 68.
  2. Kiwango cha mama wajawazito wanaoanza kliniki ya uzazi kabla ya wiki 12 za ujauzito kimeongezeka kutoka asilimia 11 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 49 katika kipindi cha Januari – Juni, 2023
  3. Kiwango cha akina mama wajawazito waliokamilisha hudhurio la 4 na zaidi katika kliniki ya wajawazito kimeongezeka kutoka asilimia 38 mwaka 2016 hadi kufikia asilimia 106,  Juni, 2023.
  4. Kwa kipindi kinachoishia Juni 2023, jumla ya akina mama 22 na watoto wachanga 70 wa umri wa siku 0 hadi siku 7 walipoteza maisha kutokana na matatizo ya uzazi ambayo ni sawa na wastani wa vifo vya akina mama 77 kwa kila vizazi hai 100,000 na vifo 2 vya watoto wachanga kwa kila vizazi hai 1,000. Hata hivyo, viwango hivyo vya vifo ni vya chini ikilinganishwa na viwango vya kitaifa ambavyo ni 556/100,000  kwa wazazi na 47/1,000 kwa watoto wachanga
  5. Vituo vya afya vinavyotoa huduma za dharura ikiwemo huduma za upasuaji wakati wa kujifungua vimeongezeka kutoka 7 mwaka 2015 hadi 16 Juni 2023.

 

3.6. Hali ya uwepo wa bidhaa za Afya na Uchunguzi.

Mkoa umeendelea kusimamia hali ya upatikanaji wa dawa, vifaatiba na vitendanishi katika vituo vyote vya kutolea huduma za Afya na kufikia mwezi Julai,2023, uwepo wa bidhaa za Afya katika vituo hivyo ni wastani wa asilimia 92% ambapo katika Manispaa Sumbawanga wana wastani wa 94% Halmashauri ya Wilaya Sumbawanga 89 % Halmashauri ya Wilaya Nkasi 91% Halmashauri ya Wilaya Kalambo 93%

3.6.1. Matumizi ya fedha za bidhaa za Afya kupitia vyanzo mbalimbali Hadi Juni, 2023.
Jedwali Na.8.Matumiz ya Fedha
Taasisi
Salio anzia
Ruzuku ya Serikali
Vyanzo vingine
Matumizi
Bakaa
Sumbawanga MC

       114,018,327.19

   1,259,961,620.68

   1,094,909,834.54

   2,472,512,050.37

     (3,622,267.96)

Sumbawanga DC

       295,089,299.42

       796,463,383.86

         84,554,781.79

       977,275,268.06

   198,832,197.01

Nkasi DC

       637,571,041.44

       806,297,472.92

         75,215,234.45

       922,752,040.48

   596,331,708.33

Kalambo DC

       168,200,623.58

       653,973,469.48

       296,052,836.04

   1,024,702,566.44

     93,524,362.66

Rukwa

   1,214,879,291.63

   3,516,695,946.94

   1,550,732,686.82

   5,397,241,925.35

   885,066,000.04

 

 

 

3.7. Mapato na Matumizi ya Fedha yatokanayo na Vyanzo mbalimbali katika Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa Mwaka 2022/2023
Jedwali Na.9. Mapato na Matumizi ya Fedhakatika Halmashauri
Halmashauri
Bajeti
Mapato
Matumizi
Bakaa
HW Kalambo
   2,037,850,156.69
   1,714,491,254.12
   1,543,919,374.36
   170,571,879.76
HW Nkasi
   3,227,719,635.18
   3,046,879,434.84
   2,690,757,328.01
   356,122,106.83
HW Sumbawanga
   2,171,003,453.79
   1,061,098,701.54
       707,833,099.58
   353,265,601.96
Sumbawanga Manispaa
   1,822,844,173.91
   1,425,018,468.28
   1,349,892,053.74
     75,126,414.54
Jumla
   9,259,417,419.57 
   7,247,487,858.78 
   6,292,401,855.69 
   955,086,003.09 
 
3.7.1. Mapato na Matumizi ya Fedha yatokanayo na Makusanyo ya ndani (NHIF, DRF, UF, ICHF) katika Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa Mwaka 2022/23
Jedwali Na.10.Mapato na Matumizi kwa fedha za ndani
Halmashauri
Bajeti
Mapato
Matumizi
Bakaa
HW Kalambo
       220,582,212.05
       728,225,517.35
       679,224,251.89
     49,001,265.46
HW Nkasi
       550,974,183.32
       622,262,093.80
       516,377,526.19
   105,884,567.61
HW Sumbawanga
       240,760,335.91
       253,239,759.06
       109,586,428.02
   143,653,331.04
Sumbawanga Manispaa
       211,554,460.36
       131,494,295.19
       114,066,195.90
     17,428,099.29
Jumla
   1,223,871,191.64 
   1,735,221,665.40 
   1,419,254,402.00 
   315,967,263.40 
 
3.7.2. Mapato na Matumizi ya Fedha za HSBF katika Vituo vya kutolea huduma za Afya kwa Mwaka 2022/23
Jedwali Na.11.Mapato na Matumiz kwa chanzo cha HSBF
Halmashauri
Bajeti
Mapato
Matumizi
Bakaa
HW Kalambo
       980,147,999.59
       571,357,833.54
       531,760,478.07
     39,597,355.47
HW Nkasi
       468,954,010.15
       610,832,756.54
       506,081,654.56
   104,751,101.98
HW Sumbawanga
       585,300,315.88
       668,198,929.46
       470,727,908.56
   197,471,020.90
Sumbawanga Manispaa
       563,433,262.84
       300,538,954.75
       252,783,588.11
     47,755,366.64
Jumla
   2,597,835,588.46 
   2,150,928,474.29 
   1,761,353,629.30 
   389,574,844.99 
  • CHANGAMOTO.

Uhaba wa magari kwa ajili ya shughuli za usimamizi na usambazaji wa bidhaa za afya katika ngazi ya Mkoa na Halmashauri.

Uhaba wa watumishi wenye ujuzi katika vituo vya kutolea huduma.

Uchelewaeshaji wa fedha kutoka serikali kuu katika ngazi ya Halmashauri na vituo vya kutolea huduma.

Uchache wa wadau wa maendeleo katika sekta ya Afya.

Baadhi ya vituo vya Afya vilivyokamilika kutokutoa huduma kwa sababu ya uhaba wa vifaa tiba.

5.0. MIKAKATI

Kushauri na kusimamia Halmashauri kutenga bajeti na kuomba vibali mbadala kwa watumishi wataalam kwa kada zenye uhitaji mkubwa.

Kuomba vyombo vya usarifi mfano magari na boti za kubebea wagonjwa.

Kuhakikisha vituo vinavyokamilika vinakuwa na watumishi na vifaa tiba vya utoaji wa huduma.

Kuwepo kwa mpango wa mafunzo kazini kwa ajili ya kuwaendeleza kitaaluma wataalam wa afya.

Kuendelea kusimamia mpango wa mkoa wa udhibiti wa magonjwa ya mlipuko.


Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa