• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kilio cha Wananchi nane nane ya Kimkoa chasababisha agizo la RC Rukwa.

imewekwa Tar: August 6th, 2017

Wananchi wa Halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa wamemuomba mkuu wa Mkoa huo kamishna Mstaafu Zelote Stephen Kufanya maonyesho ya Nane nane Kimkoa ili wakulima na wafugaji wasioweza kufika katika ngazi ya kanda wapate fursa ya kuelimika na kuonesha bidhaa zao Kimkoa.

Maombi hayo yametolewa na wananchi wa Manispaa hiyo baada ya Mh. Zelote Stephen kutembelea mabanda kadhaa ya maonesho ya nanenane yaliyofanyika katika Manispaa hiyo kwenye kituo cha kilimo katika Kijiji cha Katumba azimio ili kutoa fursa kwa wakulima na wafugaji wadogo kuonyesha bidhaa zao.

“mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wanaokwenda kwenye maonyeshoi ya nanenane kanda ni wachache sana na wengi tuliopo hatuna vipato vya kutosha kutufikisha huko, hivyo tunaomba tufanye nane nane ya Kimkoa ili nasi tuweze kuonyesha bidhaa zetu na tuweze kujifunza kwa wenzetu,” Alisema Pscal Mwanisawa Mkulima wa Kijiji cha Ulinji Manispaa ya Sumbawanga.

Kuwepo kwa maonyesho hayo ni utekelezaji wa pendekezo la Mh. Zelote aliyetaka kila halmashauri kufanya maonesho ili wakulima na wafugaji waweze kuelimishana na kutambulika katika maeneo yao ili wapate msaada kutoka kwa maafisa ugani ili kuongeza tija katika kilimo na ufugaji na hatimae kuongeza thamani katika mazao yao.

Akipokea maombi hayo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amesema kuwa ili wananchi waweze kujikwamua ni muhimu kuungana na kuwa na utambulisho wa aina moja wenye bidhaa tofauti katika makundi yao ili kuwa na nguvu.

“Muitikio wa wakulima na wafugaji katika Mkoa wa Rukwa upo juu sana, ila hawapewei nafasi, sasa mwakani ni lazima kwa Halmashauri zote kufanya nane nane katika Halmashauri zao. Nitasimamia kila mtu apate nafasi ili kujifunza teknolojia mpya na tuachane na mambo ya zamani,” Mh. Zelote alisema.

Katika kuunga mkono ombi la wananchi hao Mbunge wa Viti maalum Mh. Silafi Maufi, alipongeza juhudi za Mh. Zelote kwa kuhakikisha wananchi wa Halmashauri wanapata nafasi ya kuonesha bidhaa zao mbali na kuongeza kuwa ni jambo linalowezekana kufanya “Nane nane” ya kimkoa.

“ mheshimiwa mkuu wa Mkoa umekuwa shahidi kwa namna maonyesho yalivyofana ni Dhahiri kuwa inawezekana kufanya nane nane ya kimkoa katika mkoa wetu wa Rukwa,” Mh. Maufi alimalizia.

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza Mkoa wa Rukwa 2018 January 05, 2018
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Kikao cha Road Board Mkoani Rukwa October 08, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wagombea 1,851 wa vyama vya upinzani kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa Mkoani Rukwa.

    November 23, 2019
  • Agizo la Rais Dkt. John Pombe Magufuli latekelezwa kwa asilimia 100 Sumbawanga

    November 21, 2019
  • Waziri Mkuu Mstaafu Mizengo Pinda awataka watumishi Rukwa kupambana na udumavu.

    November 20, 2019
  • Jaji Mkuu awaagiza viongozi wa Mahakama kusimamia usajili wa kesi mitandaoni

    November 14, 2019
  • Angalia Zote

Video

Kisa Kamili cha Mama Mjamzito Kujijeruhi tumboni chafafanuliwa na RMO Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa