• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo atoa wito kwa Wasanii na timu za mpira kutembelea maporomoko ya Kalambo.

imewekwa Tar: March 16th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo ametoa wito kwa wasanii mbalimbali nchinipamoja na timu za mpira wa miguu kujenga utamaduni wa kufanya utalii wa ndani ikiwemo kutembelea maporomoko yam to Kalambo, yaliyopo katika hifadhi ya mto Kalambo, Wilayani kalambo.

Amesema kuwa kwa muda mrefu maporomoko hayo yamesahauliwa na wananchi waliomo nchini hivyo ni wakati muafaka kuanza kuyatangaza maporomoko hayo ili yaweze kufahamika na wananchi wa ndani na wa nje na matokeo yake Mkoa utambulike na kuliingizia taifa mapato.

“Natoa wito kwa wasanii mbalimbali waje wachukue picha kwenye mandhari hii watangaze utalii wa nchi yetu na utalii katika Mkoa wetu wa Rukwa, Rukwa sasa hivi imefunguka kuna maandalizi ya ujenzi wa uwanja wa ndege mkubwa kule Kisumba, uwanja huo ukishajengwa bila ya shaka eneo hili litakuwa linachanganya sana katika utalii na nchi yetu itaboreka katika uchumi, mara ya mwisho ilikuja timu ya Simba ikaishia Sumbawanga naziomba timu zote za ligi kuu kuja kuyaona maporomoko ya kalambo” Alisema

Kwa upande wake Kaimu meneja wa Wakala Huduma za Misitu (TFS) Wilayani Kalambo Chesco Lunyungu amesema kuwa wamejitahidi kufungua njia inayofika hadi chini ya maporomoko hayo jambo ambalo kwa upande wa Zambia hawawezi kufika chini maji yanapomwagika hivyo kwa kupitia mkandarasi Green Civil and Construction Ltd, tayari ngazi yenye urefu wa mita 217 imeshajengwa ili kuweka mazingira mazuri ya watalii kuweza kufika pale maji yanapoagukia ujenzi ambao umekamilika kwa asilimia 95.

Ameongeza kuwa ujenzi huo umegharimu Shilingi milioni 76 huku ujenzi huo ukiendelea ambapo hadi kukamilika kwake kunahitajika Shilingi Bilioni 1, tofauti na ngazi hizo pia kuna njia za kuchonga zenye urefu wa mita 500 za kumuwezesha mtalii kufika eneo la maji yanapomwagika pamoja na kuandaa maeneo mawili ya kupumzikia watalii “Campinga Site”

“Maporomoko haya yana urefu wa mita 235 na ni ya pili kwa ukubwa katika afrika na pia vivutio vilivyopo ni vya pili kwa uzuri katika bara la Afrika ambavyo ni pamoja na muda wote kuwa na upinde wa mvua “rainbow” pale maji yanapoanguakia ambao watalii wanavutiwa sana, pamoja na uoto wa asili unaopatikana chini ya maporomoko hayo.” Alisema.

Maporomoko hayo yanapatikana katika hifadhi ya mto Kalambo, yenye ukubwa wa hekta 534.9 mpakani mwa Tanzania na Zambia ambayo yapo chini ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) yenye urefu wa mita 235.

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa