• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Zao la Ngano kuwa mkombozi wa wakulima Rukwa.

imewekwa Tar: November 22nd, 2018

Jukwaa la Ngano Rukwa (JUNGARU) kwa kushirikiana na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Uyole Mkoani Mbeya wamefanya Mkutano na wadau wa zao la ngano Mkoa humo ukiwa na lengo la kujadili na kuinua Kilimo cha zao hilo ili kuweza kumkomboa mkulima kwani soko la zao hilo ni kubwa ndani na nje ya nchi ukilinganisha na zao la mahindi ambapo wakulima wengi wamekuwa wakilima nakukosa soko la uhakika.

Katika Kuhakikisha jambo hilo linafanikiwa mkutano huo uliambatana na uzinduzi wa wa mradi wa Kilimo cha ngano uitwao Technologies for African Agriculture Transformation (TAAT) wenye lengo la kuunga mkono na kuhakisha Kilimo cha ngano ndani ya mkoa kinakuwa chenye tija ili kusaidia kuongeza wigo wa mazao ya biashara.

Mkuu wa Mkoa wa rukwa Mh. Joachim Wangabo ambaye alikuwa mgeni rasmi wa mkutano huo alisema kuwa Mkoa wa Rukwa ni miongoni mwa mikoa inayozalisha kwa wingi zao la mahindi na kuongeza kuwa imefika wakati sasa kuwahimiza wakulima hao kulima zaidi mazao ya kibiashara ikiwemo zao la alizeti, kahawa na ngano.

“Mradi huu ambao lengo lake ni kuongeza tija katika uzalishaji wa ngano hadi kufikia tani 3.5 kwa hekta moja, hii inaonyesha ni jinsi gani serikali yetu kupitia taasisi hii inadhamira ya dhati kuhakikisha kuwa kilimo cha ngano kinakuwa cha tija katika soko letu, mahitaji ya ngano ni makubwa kufikia tani 1,000,000 ambapo kwa sasa uzalishaji ni tani 100,000 tu, hivyo ongezeko la uzalishaji litasaidia serikali kupunguza matumizi ya fedha nyingi za kigeni kuagiza ngano nje ya nchi,” Alibainisha.

Akishukuru ushirikiano anaoupata kutoka katika ofisi ya mkuu wa mkoa Mwenyekiti wa JUNGARU Mama Mzindakaya alisema kuwa ushauri alioupata kutoka kwa Mh. Wangabo wa kusajili jukwaa hilo na kuwa chama cha ushirika wamelifanyia katika na hivyo wapo katika hatua za mwisho ili kuweza kukamiliza usajili katika wizara ya mambo ya ndani na kuongeza kuwa zao la ngano ni moja ya mazao rahisi kuyalima.

Wakati akiutambulisha mradi huo mratibu wa mradi huo kutoka Ethiopia Solomon alisema kuwa bara la afrika linatumia pesa nyingi sana katika kuagiza chakula kutoka nje ya afrika na hivyo imefika wakati sasa waafrika kuanza kujitegemea katika kuzalisha chakula cha kutosha na hatimae kuweza kutumia fedha hizo kwa maendeleo mengine.

Katika Mkutano huo maazimio yaliyofikiwa ni pamoja na Kila Wilaya kuwa na wakulima wa ngano wasiopungua 300 kufikia tar 30 Desemba, 2018. Wakulima wa ngano wachange fedha kwa ajili ya kununua Mbegu kulingana na uhitaji wake ili ikanunuliwe Uyole Mbeya kufikia 30 Desemba, 2018. Mradi wa TAAT kufanya mafunzo ya Kilimo bora cha ngano kwa wakulima wa ngano kila Wilaya, mafunzo yatahusu pia ujasiriamali, pamoja na ushirika

Matangazo

  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • UTARATIBU WA UOMBAJI WA VITAMBULISHO VYA UJASILIAMALI March 24, 2021
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Wafanyabiashara waombwa kuwa na huruma na wanaofunga mwezi wa Ramadhan

    April 16, 2021
  • Stendi Kuu ya Mabasi Sumbawanga kufunguliwa mwezi Mei

    April 15, 2021
  • Mwamko mdogo wa Wananchi wakwamisha zoezi la Urasimishaji Makazi Sumbawanga

    April 14, 2021
  • Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

    April 05, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa