• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

DC NKASI ATOA SIKU 7 WATOTO WOTE KURIPOTI KIDATO CHA KWANZA

imewekwa Tar: January 19th, 2021

MKUU wa Wilaya ya Nkasi mkoani Rukwa Mh.Said Mtanda ametoa siku saba kwa wanafunzi wote 1,641 kujiunga Kidato cha Kwanza katika shule walizopangiwa.

Alisisitiza kuwa Walimu Wakuu wawapokee wanafunzi hao hata kama hawana sare za shule na kutembea peku .

"Wabunge,madiwani,wataalamu,maofisa elimu kata, maofisa tarafa,watendaji wa vijiji na kata pia Ofisa Elimu Elimu ya Msingi Wilaya wahakikishe wazazi na walezi watoto wao wanaripoti shuleni kwa wakati vinginevyo hatua kali zitachukuliwa dhidi yao" alieleza.

Alisema wanafunzi hao 1,641 ambapo hawajajiunga na Kidato cha Kwanza katika shule walizopangiwa wilayani humo tangu zifunguliwe Januari 11,mwaka huu ni sawa na asilimia 40 ya wanafunzi 4,301 waliochaguliwa.

Mtanda alitoa maelekezo hayo alipokutana na wanahabari na kuzungumzia kufunguliwa kwa shule za msingi na sekondari na wanafunzi walioripoti Kidato cha Kwanza wilayani humo.

"Wanafunzi hao 1,641 kabla ya mwisho wa siku hii wawe wameripoti katika shule walizopangiwa ili waajiriwe katika mfumo ambao una muda maalumu...

Serikali imeelekeza wanafunzi wanaojiunga Kidato cha Kwanza wote wasajiliwe katika mfumo......

Katika wilaya hii kati ya wanafunzi 4,301 waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza wanafunzi 2,660 sawa na asilimia 60 wameripoti katika shule walizopangiwa na 2,582 wamesajiliwa katika mfumo"alieleza.

Kuhusu miundombinu ya vyumba vya madarasa amesema wilaya hiyo haina changamoto ya upungufu wake kwa kuwa mwaka uliopita maboma 560 ya shule za msingi na sekondari ujenzi wake ulikamilika.

Kwa upande wa samani alisema kuwa wilaya hiyo ilikuwa na upungufu wa madawati,viti na meza 5,621.

"Ili kukabiliana na upungufu huo viti 473 na meza 516 vilivyokuwa vimeharibika,vimekarabatiwa na kusambazwa katika shule 28 za sekondari pia kila shule ya sekondari imeelekezwa kutengeneza viti na meza 20"alisema.

Akiongeza kuwa " Miti iliyoanzishwa wakati wa ukarabati wa barabara ya Wampembe imechanwa na zimepatikana mbao 650 ambapo vimetengenezwa viti na meza 500 na kusambazwa katika shule zenye mahitaji" alibainisha.

Matangazo

  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • HOTUBA YA BAJETI YA TAMISEMI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2024 May 05, 2023
  • Bei ya Mbolea za Rukuzu kwa Wakulima August 31, 2022
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MIRADI YA BILIONI 56.7 YAKAGULIWA KALAMBO

    September 25, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WITO KWA WAZAZI KUHAKIKISHA WATOTO WANAPATIWA CHANJO

    September 21, 2023
  • WAAGIZWA KUKAMILISHA MAANDALIZI YA CHANJO POLIO

    September 15, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa