• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Waziri Tizeba aagiza wanaouza mbegu feki wafungiwe maduka yao

imewekwa Tar: November 29th, 2017

Waziri wa Kilimo Mh. Charles Tizeba ameiagiza Taasisi ya Uthibitishaji Rasmi wa Mbegu Tanzania (TOSCI) kufanya ukaguzi wa duka kwa duka kwenye maduka ya wafanyabiashara wa pembejeo ili kuwabaini wanaouza mbegu feki na na kuwafungia biashara zao ikibainika wanafanya hivyo.

Amesema kuwa kuwa suala la mbegu feki linawakatisha tamaa wakulima ambao wanategemea kilimo kwaajili ya kuendesha maisha yao na kuwa serikali ya awamu ya tano haitalivumilia jambo hilo na itaendelea kumtetea mkulima nae afaidike kwa kazi anayoifanya.

“Mkulima badala ya kupata gunia 15 hadi 20 anaambulia gunia tano na wananchi wengi hawana uwezo wa kugundua kwamba kinachomsababisha asivune ni mbegu feki, yeye atadhani labda ni hali ya hewa kumbe ni mwizi mmoja kwa tamaa zake amekwamisha maendeleo ya mkulima huyu,” Mh. Tizeba alisisitiza.

Ameyasema hayo alipotembelea shamba la msipazi lililopo katika Kijiji cha china, Wilayani Nkasi na kulalamikiwa na mmiliki wa shamba hilo Salum Sumry aliyeuziwa mbegu feki na Johanes Sanga mwenye duka linaloitwa Gadu Store na kumfungulia kesi mahakamani, kesi ambayo inaendelea hadi leo.

Mh. Tizeba amesema kuwa kesi hizo hazifai kuendeshwa na mkulima badala yake watu wa TOSCI wanatakiwa kuingilia kati ili kupambana na wauzaji hao wa mbegu feki ili kulimaliza tatizo hilo.

Aidha, Waziri Tizeba ameagiza watu wa udhibiti wa mbolea kushughulikia suala la bei elekezi katika mbolea kuhakikisha maduka yote ya pembejeo nchini wanabandika mabango ya bei elekezi za mbolea nje ya maduka yao ili kila mkulima na mnunuzi aweze kuelewa bei hizo na kuongeza kuwa bei hizo elekezi ni kwaajili ya mnunuzi wa mwisho kijijini na sio makao makuu ya Mkoa au Wilaya.

“Huu mzaha wa bei elekezi kuuzwa kwa jumla Mkoani au Wilayani likome, wafuatilie watu waweke matangazo kwenye maduka yao, kwamba bei za Mkoani na Wilayani sio zile zilizotangazwa za mkulima, hizo za mkulima ni kijijini ndipo ananunua ile bei iliyotangazwa na serikali, sio Namanyere kule anatakiwa kuuza chini yah apo,” Mh. Tizeba alifafanua.

Kwa upande wake kaimu Mkurugenzi Mamlaka ya Udhibiti wa Mbolea Tanzania (TFRA) Lazaro Kitandu amefafanua kuwa mfumo ulioanzishwa na serikali wa ununuzi wa mbolea kwa pamoja unarahisisha upatikanaji wa mbolea nyingi kwa wakati mmoja na hivyo mbolea kuwa na bei ya chini.

“Mfumo huu unadhibiti ununuzi wa mbolea kutoka kwenye chanzo usafirishaji wake, gharama za bandari, gaharama za usafirishaji ndani ya nchi na ile faida anayotaka kuweka mfanyabiashara, kwahiyo hakuna tena nafasi kwa mfanyabiashara kujiongezea bei pasipokjuwa na uhalali, hakuna tena kumnyonya mkulima pasipo halali,” Kitandu alifafanua.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa