• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Huduma ya Elimu

Sekta ya Elimu

Azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ni kuhakikisha kila Mtoto anayestahili kupata Elimu Msingi (Basic Education) anapata Elimu hiyo.  Mpango wa Serikali wa Elimu Msingi bila malipo umekuwa na mafanikio makubwa.  Mafanikio hayo ni pamoja na;-

  • Asilimia ya uandikishaji wa  darasa la kwanza umeongezeka kutoka 40,404 mwaka 2016 hadi  50,887 sawa na ongezeko la 26% mwaka 2018.
  •  Idadi ya Wanafunzi wa kidato cha I-VI imeongezeka  kutoka 25,241 mwaka 2016  hadi kufikia 33,723  mwaka 2018. Hii ni sawa na ongezeko la 34%.
  • Idadi ya shule zenye Kidato cha Tano na Sita zimeongezeka kutoka 10 (Mwaka 2016) hadi kufikia 15 (Mwaka 2018). Hii ni sawa na ongezeko la 50%.
  • Kipindi cha Mwaka 2017-2018 Serikali imetoa kwa Mkoa Jumla ya Shilingi 5,114,012,715.00 za elimu bila malipo kwa shule za Msingi na Sekondari ikiwa ni fedha kwa ajili ya Ruzuku (Capitation Grant), fedha ya chakula, posho ya waratibu elimu Kata, posho ya walimu wakuu, wakuu wa shule na fidia ya ada.

Mafanikio Kitaaluma:

Matokeo ya Mitihani Mwaka 2017/2018

Mkoa umeendelea kusimamia suala la Elimu kikamilifu. Aidha, katika upimaji wa Mitihani ya kitaifa matokeo ya ufaulu yamekuwa yakiongezeka kama ifuatavyo;

  • Matokeo ya darasa la Nne

Matokeo ya mtihani wa upimaji kwa Darasa la Nne yameendelea kuimarika  kutoka ufaulu  wa aslimia 88.00 kwa mwaka 2016  hadi asilimia 89.11  kwa mwaka 2017 .

  • Matokeo ya Darasa la Saba, 2017

Matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi yanaonesha kupanda kwa ufaulu wa wanafunzi kutoka ufaulu wa 66% kwa mwaka 2016 hadi 68.05% kwa mwaka 2017.  Kulingana na Tathmini ya mtihani wa utimilifu ufaulu unatarajia kuongezeka hadi kufikia asilimia 78% kwa mwaka 2018.

Idadi ya Wanafunzi waliofaulu 12,867 wote walichaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza 2018. Kati yao Wanafunzi 54 shule za bweni na 12,813 shule za kutwa. Wanafunzi hao wote walipatiwa nafasi za kuendelea na masomo.

  • Matokeo ya kidato cha pili

Katika mtihani wa upimaji Kidato cha Pili mwaka, 2017, ufaulu wa wanafunzi uliongezeka kutoka asilimia 87.6 mwaka 2016 hadi  asilimia 92.08 kwa mwaka 2017. 

  • Matokeo ya kidato cha Nne

Matokeo ya mtihani wa Kidato cha Nne mwaka 2016, Mkoa ulishika nafasi ya 12 kitaifa kati ya Mikoa 31 ukilinganisha na mwaka 2017 ambapo Mkoa ulishika nafasi ya 13. Aidha Jitihada za ufundishaji, ufuatiliaji na usimamizi zimefanyika ili kwa mwaka 2018 Mkoa uwe katika nafasi nzuri zaidi kitaifa.

  • Matokeo ya kidato cha Sita

Matokeo ya mtihani wa Kidato cha Sita mwaka 2017 Mkoa ulishika nafasi ya 8 kitaifa kati ya Mikoa 29 ukilinganisha na mwaka 2018 ambapo Mkoa ulishika nafasi ya 13. Aidha, jitihada za ufundishaji, ufuatiliaji na usimamizi zinaendelea kufanyika ili kwa mwaka 2019 Mkoa uweze kushika nafasi nzuri zaidi kitaifa ukilinganisha na mwaka huu.

Utekelezaji wa miundombinu ya elimu Mkoa

  • Serikali inaendelea na jitihada za kuboresha miundombinu mbalimbali ya elimu kama ifuatavyo;
  • Miundo mbinu ya Maabara

Katika kipindi cha mwaka 2015 tulikuwa na maabara 24, na kwa mwaka 2018 maabara zimeongezeka hadi kufikia maabara 31. Aidha, maabara 177 zinaendelea kujengwa katika Mkoa wetu ambazo zipo katika hatua mbalimbali za ujenzi.

  • Vyumba vya Madarasa

Katika kipindi cha mwaka 2015 Vyumba vya madarasa vilivyokuwepo kwa shule za msingi na Sekondari ni 3,140 na kwa mwaka huu wa 2018 vyumba vya madarasa vimeongezeka hadi kufikia 3,329.

  • Nyumba za Walimu:

Katika kipindi cha mwaka 2015 nyumba za walimu wa shule za msingi na Sekondari zilikuwa ni 1,955 na kwa mwaka 2018 zimeongezeka hadi kufikia nyumba 2,124.Ongezeko hili ni jitihada za serikali kuendelea kuboresha miundombinu ya elimu kwa walimu.

  • Matundu ya Vyoo

Katika kipindi cha mwaka 2015 matundu ya vyoo yalikuwepo ni 4,391 na kufikia mwaka 2018 matundu ya vyoo yameongezeka kufikia 5,438.

  • Madawati:

Serikali imeendelea na jitihada za kuboresha sekta ya elimu kwa kuhakikisha madawati yanatengenezwa mashuleni. Aidha, katika kipindi cha mwaka 2015/2016 tulikuwa na madawati 37,311 kwa shule za msingi, meza 21,757 na viti 22,093 kwa shule za Sekondari. Aidha, kwa mwaka 2018 madawati yameongezeka kufikia 80,501 kwa shule za msingi, meza na viti 33,686 kwa sekondari  kufikia mwaka huu 2018.

  • Mimba kwa Wanafunzi 
  • tatizo la mimba kwa wanafunzi wanaosoma Elimu ya Msingi na Sekondari ni kubwa. Kuanzia Julai 2017 hadi Mei, 2018 jumla ya wanafunzi 121 wamepata ujauzito, kati ya hao wanafunzi wa Elimu ya Msingi ni 46 na wa Elimu ya Sekondari ni 75. Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na Watendaji wa Kata kufikisha kesi hizo Polisi na Mahakamani kwa ajili ya hatua zaidi.  Mpaka sasa matukio yote 121 yameripotiwa Polisi kwa ajili ya hatua za kisheria.
  • Ili kukabiliana na tatizo la mimba mikakati mbalimbali imewekwa ikiwemo ifuatayo;
  • Kutoa elimu kwa jamii pamoja na wanafunzi hasa wakike juu ya hasara za kupata mimba wakati bado ni mwanafunzi ili waone umuhimu wa kuacha tabia hiyo.
  • Chakula kwa wanafunzi ambapo hamasa kwa wazazi na kamati za shule imetolewa kuhakikisha wanafunzi wanapata chakula shuleni.
  • Ujenzi wa Hosteli za wasichana kwenye shule za Sekondari za Kata ambapo jumla ya Hosteli 54 zimejengwa.
  •  Kushirikiana na mahakama ili wahusika wanaojihusisha na kuwapa mimba wanafunzi wachukuliwe adhabu kali kisheria.

Ujenzi wa chuo cha VETA Sumbawanga

 

Tarehe 31/08/2018 VETA Makao Makuu Dar es Salaam, VETA Kanda ya Nyanda za Juu Kusini Mbeya pamoja na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa tulifanya hafla fupi ya kumkabidhi Mkandarasi TENDER INTERNATIONAL kiwanja kwa ajili ya kuanza ujenzi wa Chuo Cha Ufundi Stadi (VETA) katika Manispaa ya Sumbawanga pamoja na Mkandarasi, Mshauri Elekezi (Consultant) Sky Architect Consultancy Ltd.

Eneo hilo ambalo VETA itajengwa lipo Kashai (MUVA) katika Manispaa ya Sumbawanga na lina ukubwa wa 95,934 sq M Plot 1 Block ‘A’ (LD) chenye hati Namba 44102-MBYLR iliyotolewa tarehe 5 Machi, 2018.

Mradi unategemewa kukamilika ndani ya miezi 12 (kuanzia tarehe ya makabidhiano). Aidha, gharama za ujenzi za mradi huu ni Tsh. 10,700,488,940.05. Ujenzi ukikamilika chuo kitaweza kuchukua wanafunzi 900 wa kozi ndefu na 600 wa kozi fupi hivyo, kitakuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya wanafunzi 1,500.

Matangazo

  • Matokeo ya Kidato cha SITA 2018 July 16, 2018
  • Matokeo ya Darasa la 7 mwaka 2018 Mkoani Rukwa. October 23, 2018
  • WATAHINIWA WALIOFAULU KWA NAFASI YA SHULE ZA KUTWA MWAKA 2019 MKOA WA RUKWA December 17, 2018
  • Waliochaguliwa kujiunga Kidato cha Kwanza Mkoa wa Rukwa 2018 January 05, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC Wangabo Kupita Kijiji hadi Kijiji kuwasaka wajasiliamali wasio na vitambulisho.

    February 04, 2019
  • Wajasiliamali wasiotambulika wapewa wiki tatu kujisalimisha

    February 01, 2019
  • Shule ya kata iliyoachwa kwa miaka 10 kusajiliwa mwaka huu Rukwa.

    January 23, 2019
  • Wanaowinda panya washauriwa kufuga kuku ili kupunguza uharibifu wa mazingira.

    January 21, 2019
  • Angalia Zote

Video

RC Wangabo azihamasishaTaasisi na wananchi kufika Msitu wa mbizi kuchukua miti.
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

Wapitiaji

https://www.stat-counter.org

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa