• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

imewekwa Tar: February 18th, 2021

WANAFUNZI 6 wa shule mbalimbali za msingi wilayani Nkasi mkoani Rukwa wamefariki jana jioni ambapo Wanne walipigwa na radi na wawili kugongwa na gari katika maeneo tofauti,ambapo watatu kati ya waliopigwa na radi ni wa familia moja.

Akizungumza kwenye mazishi ya Watoto Watatu wa familia moja katika kijiji cha Nkana kata ya Nkandasi mkuu wa wilaya Nkasi Mh. Said Mtanda alisema kuwa wilaya Nkasi ina majonzi makubwa ambapo jana tu ni watoto 6 wamepoteza maisha ambapo Wanne walipigwa na radi na wawili kugongwa na gari katika maeneo tofauti.

Alisema kuwa vifo hivyo vimeleta simanzi kubwa wilayani Nkasi na kuwaomba Wananchi kuondoa fikra zozote mbaya juu ya vifo hivyo kwani yote ni mapenzi ya Mungu.

Awali kaimu afisa elimu wa wilaya Agnes Martin alisema kuwa licha ya Watoto watatu wa familia moja kuuawa kwa radi katika kijiji hicho cha Nkana pia kuna mwanafunzi mwingine wa shule ya msingi Nchenje naye alipigwa na radi wakati Wanafunzi wengine Wawili waligongwa na gari.

Aliwataja Watoto hao wa familia moja waliofariki kuwa ni Rita Remi Chiwalala (6) Mwanafunzi ya awali katika shule ya msingi Nkana,Macrida Chrisipine Mtepa (7) darasa la 1 na Exavery Lucas Chipamba (13) wa darasa la 5 na mwingine ni Kwilasa Siri (9) wa darasa la tatu shule ya msingi Nchenje ambaye alipigwa na radi jioni akiwa nyumbani kwao.

Pia aliwataja Wanafunzi wengine waliofariki kwa kugongwa na gari ni Boniphace Regius Sapi (8) wa darasa la pili shule ya msingi Kipundukala na Debora Chulula (12) darasa la tatu shule ya msingi Chala.

Akisimulia mkasa huo kaimu afisa elimu kata ya Sintali Patrick Fute alisema kuwa radi hiyo iliyowapiga Watoto wa familia moja ilitokea majira ya saa 11 jioni walipokuwa wakicheza mchezo wa kitoto na walikua 11 na baada ya radi hiyo kushuka Watoto hao watatu walifariki papo hapo.

Na Israel Mwaisaka,Nkasi

Matangazo

  • Matokeo ya Darasa la Saba 2019 - Rukwa October 17, 2019
  • Orodha ya Wanafunzi Waliochaguliwa Kujiunga Kidato cha Kwanza Mwaka 2021, Mkoa wa Rukwa December 18, 2020
  • Fomu za Kujiunga na Shule mbalimbali za Sekondari (JOINING INSTRUCTION) kwa Mwaka 2021 mkoani Rukwa. December 20, 2020
  • Kikao cha Kamati ya Ushauri ya Mkoa (RCC) October 09, 2018
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • Waliokula Shilingi Milioni 932 za Halmashauri kufikishwa mahakamani.

    February 24, 2021
  • Wajumbe RCC waiomba Serikali kuhuisha Mradi wa VETA Sumbawanga ili kuwakomboa Wananchi.

    February 23, 2021
  • Shughuli za kibinadamu bado ni Changamoto katika uharibifu wa madaraja na barabara

    February 22, 2021
  • SITA WAFA KWA MATUKIO TOFAUTI IKIWEMO RADI

    February 18, 2021
  • Angalia Zote

Video

Mwaka 2020 kuwa mwaka wa kuwalinda watoto dhidi ya Ukatili Mkoani Rukwa
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Regional Block, 90 Mwl. Julius Nyerere Road

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0756941328

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa