Friday 9th, June 2023
@Sumbawanga
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Joseph Joseph Mkirikiti leo (01.09.2021) ameongoza kika cha Kikao cha Kamati ya Kusimamia,Kudhibiti na Kuratibu Mapato na Matumizi ya Serikali Robo ya Nne 2020/21 katika ukumbi wa mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa mjini Sumbawanga ambapo ameagiza Wakurugenzi wote wa halmashauri kushirikiana kwa karibu na Wakaguzi wa Hesabu wa Ndani ili fedha zote zinaztolewa na serikali kwa ajili ya miradi ya maendeleo ya wananchi zitumike kikamilifu.
Mkuu huyo wa Mkoa amewataka pia watendaji wa serikali kutumia sheria nakanuni za fedha katika kuhakikisha wananchi wananufaika na kodi zao kwenye kujiletea maendeleo.
Kikao hicho kimehusisha Katibu Tawala Mkoa Bw. Denis Bandisa, Wakuu wa Idara na Vitengo, Wakurugenzi wa Halmasahauri, Waweka Hazina wa Halmashauri na Wakaguzi wa Hesabu wa Ndani toka Halamashauri zote za Rukwa.
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani
Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA
Simu: 025 280 2137
Simu: 0739862632
barua pepe: ras@rukwa.go.tz
Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa