• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

imewekwa Tar: March 19th, 2025

JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE


Jamii imeaswa kujenga utamaduni wa kuwaheshimu na kuwahudumia wazee badala ya kutegemea tu sheria zilizopo, kwani bila mtazamo chanya wa kijamii, juhudi za serikali hazitakuwa na mafanikio ya kudumu.


Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Ndg. Hajjayand Adon, wakati akifungua kikao cha Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Rukwa, kilichofanyika tarehe 19 Machi 2025, katika Ukumbi Mdogo wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.


Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa amesema kuwa mahitaji ya wazee wengi ni ya msingi na yanaweza kutatuliwa na jamii endapo utamaduni wa kuwahudumia wazee utajengwa kwa dhati. Amesisitiza kuwa wazee wengi ni wale waliotulea na kutufikisha hapa tulipo, na kwa umri wao, mahitaji yao makubwa ni chakula, malazi na matibabu, ambayo gharama yake si kubwa kwa jamii.


Ameeleza kuwa bila jamii kubadili mtazamo na kuendeleza utamaduni wa kuwaheshimu na kuwahudumia wazee, sheria pekee hazitakuwa na tija katika kuhakikisha ustawi wa wazee.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Rukwa, Ndg. Timoth Makaza, amesema kuwa licha ya uwepo wa sera na sheria za kusaidia wazee, bado kuna haja ya kuziboresha na kuhakikisha utekelezaji wake unawanufaisha wazee kwa uhalisia.


Naye Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa wa Rukwa, Ndg. Godfrey Mapunda, amesema kuwa hadi sasa mkoa umefanikiwa kutoa vitambulisho vya matibabu bila malipo kwa wazee 19,994, sawa na asilimia 58 ya wazee waliotambuliwa. Hatua hii ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha wazee wanapata huduma za afya kwa urahisi na bila gharama.


Serikali na wadau wa maendeleo wamehamasishwa kuendelea kuwekeza katika sera bora na mipango madhubuti itakayohakikisha maisha bora kwa wazee, huku jamii ikihimizwa kushiriki kikamilifu katika kuwatunza na kuwaheshimu wazee kwa vitendo

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa