• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

imewekwa Tar: March 19th, 2025

JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE


Jamii imeaswa kujenga utamaduni wa kuwaheshimu na kuwahudumia wazee badala ya kutegemea tu sheria zilizopo, kwani bila mtazamo chanya wa kijamii, juhudi za serikali hazitakuwa na mafanikio ya kudumu.


Hayo yamesemwa na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Rukwa, Ndg. Hajjayand Adon, wakati akifungua kikao cha Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Rukwa, kilichofanyika tarehe 19 Machi 2025, katika Ukumbi Mdogo wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.


Akizungumza katika kikao hicho, Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa amesema kuwa mahitaji ya wazee wengi ni ya msingi na yanaweza kutatuliwa na jamii endapo utamaduni wa kuwahudumia wazee utajengwa kwa dhati. Amesisitiza kuwa wazee wengi ni wale waliotulea na kutufikisha hapa tulipo, na kwa umri wao, mahitaji yao makubwa ni chakula, malazi na matibabu, ambayo gharama yake si kubwa kwa jamii.


Ameeleza kuwa bila jamii kubadili mtazamo na kuendeleza utamaduni wa kuwaheshimu na kuwahudumia wazee, sheria pekee hazitakuwa na tija katika kuhakikisha ustawi wa wazee.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Wazee Mkoa wa Rukwa, Ndg. Timoth Makaza, amesema kuwa licha ya uwepo wa sera na sheria za kusaidia wazee, bado kuna haja ya kuziboresha na kuhakikisha utekelezaji wake unawanufaisha wazee kwa uhalisia.


Naye Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa wa Rukwa, Ndg. Godfrey Mapunda, amesema kuwa hadi sasa mkoa umefanikiwa kutoa vitambulisho vya matibabu bila malipo kwa wazee 19,994, sawa na asilimia 58 ya wazee waliotambuliwa. Hatua hii ni sehemu ya jitihada za serikali kuhakikisha wazee wanapata huduma za afya kwa urahisi na bila gharama.


Serikali na wadau wa maendeleo wamehamasishwa kuendelea kuwekeza katika sera bora na mipango madhubuti itakayohakikisha maisha bora kwa wazee, huku jamii ikihimizwa kushiriki kikamilifu katika kuwatunza na kuwaheshimu wazee kwa vitendo

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa