• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Kilio cha Wananchi nane nane ya Kimkoa chasababisha agizo la RC Rukwa.

imewekwa Tar: August 6th, 2017

Wananchi wa Halmashauri ya manispaa ya Sumbawanga Mkoani Rukwa wamemuomba mkuu wa Mkoa huo kamishna Mstaafu Zelote Stephen Kufanya maonyesho ya Nane nane Kimkoa ili wakulima na wafugaji wasioweza kufika katika ngazi ya kanda wapate fursa ya kuelimika na kuonesha bidhaa zao Kimkoa.

Maombi hayo yametolewa na wananchi wa Manispaa hiyo baada ya Mh. Zelote Stephen kutembelea mabanda kadhaa ya maonesho ya nanenane yaliyofanyika katika Manispaa hiyo kwenye kituo cha kilimo katika Kijiji cha Katumba azimio ili kutoa fursa kwa wakulima na wafugaji wadogo kuonyesha bidhaa zao.

“mheshimiwa Mkuu wa Mkoa wanaokwenda kwenye maonyeshoi ya nanenane kanda ni wachache sana na wengi tuliopo hatuna vipato vya kutosha kutufikisha huko, hivyo tunaomba tufanye nane nane ya Kimkoa ili nasi tuweze kuonyesha bidhaa zetu na tuweze kujifunza kwa wenzetu,” Alisema Pscal Mwanisawa Mkulima wa Kijiji cha Ulinji Manispaa ya Sumbawanga.

Kuwepo kwa maonyesho hayo ni utekelezaji wa pendekezo la Mh. Zelote aliyetaka kila halmashauri kufanya maonesho ili wakulima na wafugaji waweze kuelimishana na kutambulika katika maeneo yao ili wapate msaada kutoka kwa maafisa ugani ili kuongeza tija katika kilimo na ufugaji na hatimae kuongeza thamani katika mazao yao.

Akipokea maombi hayo Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen amesema kuwa ili wananchi waweze kujikwamua ni muhimu kuungana na kuwa na utambulisho wa aina moja wenye bidhaa tofauti katika makundi yao ili kuwa na nguvu.

“Muitikio wa wakulima na wafugaji katika Mkoa wa Rukwa upo juu sana, ila hawapewei nafasi, sasa mwakani ni lazima kwa Halmashauri zote kufanya nane nane katika Halmashauri zao. Nitasimamia kila mtu apate nafasi ili kujifunza teknolojia mpya na tuachane na mambo ya zamani,” Mh. Zelote alisema.

Katika kuunga mkono ombi la wananchi hao Mbunge wa Viti maalum Mh. Silafi Maufi, alipongeza juhudi za Mh. Zelote kwa kuhakikisha wananchi wa Halmashauri wanapata nafasi ya kuonesha bidhaa zao mbali na kuongeza kuwa ni jambo linalowezekana kufanya “Nane nane” ya kimkoa.

“ mheshimiwa mkuu wa Mkoa umekuwa shahidi kwa namna maonyesho yalivyofana ni Dhahiri kuwa inawezekana kufanya nane nane ya kimkoa katika mkoa wetu wa Rukwa,” Mh. Maufi alimalizia.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa