• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

MABARAZA YA ARDHI YATAJWA KUWA CHANZO CHA MIGOGORO

imewekwa Tar: January 23rd, 2021

IMEBAINIKA kuwa mabaraza ya ardhi ngazi ya vijiji na kata yamekua ni chanzo kikubwa cha migogoro ya ardhi na kuwa ipo haja kwa serikali kutizama upya mfumo huo wa mabaraza.

Hayo yamesemwa na katibu tawala wa wilaya Nkasi Cosmas Kuyela kwa niaba ya mkuu wa wilaya Nkasi Said Mtanda kwenye uzinduzi wa wiki la sheria  Nchini ambapo amesema kuwa lengo la serikali la kuweka masbaraza ni zuri lakini sasa imekuwa ni tofauti kwa wao kuwa chanzo chas migogoro mikubwa.

Alisema kuwa kupitia wiki hili la sheria Nchini ni muhimu kwa serikali kuuangalia upya mfumo huo wa mabaraza ya ardhi ya kata na ikiwezekana iangalie namna nyingine ya nabaraza kama hayo ambayo yatakua na tija kwa jamii kuliko kama ilivyo sasa.

‘’mabaraza haya ya kata na vijiji yanatupa shida sana sisi viongozi wa wilaya kwani kero imekuwa kubwa sana kwa Wananchi na ukiangalia asilimia kubwa ya kero zinazofika ofisini kwetu ni migogoro ya ardhi ambayo mingi imetokana na mabaraza ya ardhi sasa badala ya mabaraza haya kuwa mkombozi lakini sasa ndiyo yamegeuka kuwa tatizo’’alisema

Pia amebainisha kuwa matumizi ya lugha ya Kiingereza katika Mahakama ni chanzo cha wengi kukosa haki hivyo ipo haja kwa mahakama kuliona hilo ili mashauri na majalada yote ya kimahakama yaandikwe kwa lugha ya Kiswahili ambacho Watanzania wengi wanakifahamu

Alidai kuwa Wananchi ambao ndiyo walengwa wa huduma hizo za kimahakama wengi wao hawajui kabisa kiingereza na kuwa kitendo cha mahakama kutumia kiingereza katika nyaraka zao kinawaongezea gharama wananchi ya kwenda kwa Watu ili kuweza kupata tafsiri ya kile kilichoandikwa

Na aliitataka jamii kuitumia fursa hiyo ya wiki ya sheria nchini kwa kwenda kupata elimu kwa Wanasheria kitu kitakachowapelekea wao kuwa walau na uelewa wa masuala ya kisheria

Hakimu mkazi  mfawidhi wa makama ya wilaya Benedict Nkomola kwa upande wake aliwataka wananchi wote kwa ujumla kujitokeza katika wiki hili la sheria katika viwanja vya mahakama ambapo watapata elimu na kuielewa vyema idara hiyo ya mahakama inavyofanya kazi

Alisema kuwa wiki la sheria ni mwanzo wa kuanza kwa shughuli za kimahakama hapa nchini kwa mwaka huu wa 2021

Maadhimisho ya wiki la sheria mwaka huu yamebeba ujumbe usemao “miaka 100 ya mahakama kuu ;mchango wa Mahakama katika kujenga nchi inayozingatia uhuru ,haki,ududu,amani na ustawi  wa wananchi 1921-2021’’

mwisho

Na Israel Mwaisaka,Nkasi

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • MADAKTARI BINGWA 33 WAPOKELEWA RUKWA, HUDUMA ZA KIBINGWA KUTOLEWA HOSPITALI ZA WILAYA KWA SIKU TANO

    May 19, 2025
  • RUKWA YAANZA RASMI MATUMIZI YA MFUMO WA STAKABADHI GHALANI KWA ZAO LA MBAAZI NA UFUTA

    May 13, 2025
  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa