• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Matuta 212 yaliyopo barabara ya Tunduma - Sumbawanga yapatiwa ufumbuzi

imewekwa Tar: February 28th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh.Joachim Wangabo amewashauri Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoani Rukwa kukutana na madiwani pamoja na wenyeviti wa halmashauri zinazopitiwa na barabara ya Tunduma – Sumbawanga ili kuyabaini matuta yaliyowekwa maeneo ambayo hayana ulazima hivyo kutostahili kuendelea kuwepo kwenye barabara hiyo na hatimae kujiandaa kuyapunguza wakati wakiendelea kusubiri maamuzi ya Wizara.

Amesema kuwa endapo zoezi hilo litakuwa shirikishi halitazua mzozo baina ya TANROADS na wananchi pindi ajali zitakapoongezeka na kuwataka wabunge wa maeneo husika nao kukubaliana na maamuzi yatakayotolewa na wizara husika baada ya utambuzi huo wa matuta kufanyika.

“Kuna ukweli kwamba kuna baadhi ya Matuta hayastahili kuendelea kuwepo, matuta zaidi ya 200 lakini kuna baadhi yao yapo maeneo ambayo hayastahili kuwepo, mi nadhani kungefanyika utambuzi wa matuta ambayo sio ya lazima, halafu ndio hoja inakuwa kwamba kuna matuta Fulani ambayo sio ya lazima yapo katika maeneo Fulani ambayo hata waheshimiwa madiwani wa maeneo yale wameyaafiki kwasababu hii isiwe kazi ya TANROADS peke yao,”Alishauri.

Ameshauri hayo katika kikao cha Bodi ya Barabara ya Mkoa kilichowashirikisha Wakala wa Barabara nchini (TANROADS), Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA), Wakuu wa Wilaya, Wabunge, Wakurugenzi wa halmashauri pamoja na Wenyeviti wa halmashsuri za Mkoa huo.

Ushauri huo umekuja baada ya mbunge wa jimbo la Sumbawanga mjini Mh. Aeshi Hilary kuilalamikia TANROADS kuhusu wingi wa matuta hayo na matokeo yake kuwakera wasafiri wanaotumia barabara hiyo jambo ambalo limekuwa likiwachosha wasafiri wanaotoka mikoa ya mbali na Mkoa wa Rukwa.

“Utakuta kuna matuta ambayo yanawekwa sehemu ambapo wala hayastahili, barabra hii ya Tunduma – Sumbawanga ina matuta zaidi ya 240 inazidi hata kilometa za barabara yenyewe, kuna tuta lipo katikati ya daraja, kwa mfano kuna Kijiji cha Tamasenga peke yake kina matuta kumi, kuna umuhimu gani wa kuyaweka yote hayo katika Kijiji kimoja, mlisema mtayaondoa lakini hapa kwenye bajeti yenu sioni kama mmelizungumzia,” Aliuliza.

Kwa upande wake Meneja wa TANROADS Mkoani Rukwa Mhandisi Masuka Mkina alibainisha kuwa uwepo wa matuta hayo umepunguza kwa kiasi kikubwa ajali za barabarani na kuongeza kuwa wafadhili waliowezesha ujenzi wa barabara hiyo kauli mbiu yao ilikuwa ni “Usalama Kwanza”.

“Alipokuja hapa Katibu Mkuu Nyamhanga nilizungumza lakini baadae akasema tuyaache kwanza, kwahiyo suala la matuta kwa sasa mimi sina la kuzungumza kwasababu serikali bado wanaendelea kulitafakari kwamba wayatoe au yabaki, kwasababu yamesaidia sana ukiangalia takwimu kwa barabara ya Tunduma - Sumbawanga ajali nikama sifuri,” Alisema.

Barabara ya Tunduma – Sumbawanga yenye kilometa 227 inakadiriwa kuwa na matuta 212 huku madatuta kadhaa yakiwa katikati ya madaraja na Kijiji cha Tamasenga kuwa na matuta 10 imefadhiliwa kwa msaada wa watu wa Marekani imesaidia kurahisisha safari ya Tunduma kwenda Sumbawanga ambapo hapo kabla wasafiri walitumia siku nzima.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa