• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

NASIBU WAZIRI AKIRI KUWEPO CHANGAMOTO BIMA YA MFUKO WA AFYA YA JAMII

imewekwa Tar: January 5th, 2021

Na Israel Mwaisaka,Rukwa

NAIBU Waziri wa afya na ustawi wa jamii Mh. Dkt.Godwin Mollel amekiri kuwepo kwa changamoto juu ya mfumo wa Bima ya Mfuko wa Afya ya Jamii na kuwa wizara imeliona na inakwenda kulifanyia kazi.

Hilo amelisema jana alipokuwa akizungumza na Watumishi wa idara ya afya wa wilaya ya Nkasi kwenye jengo jipya la hospitali ya wilaya baada ya kupata malalamiko kutoka kwa mbunge wa jimbo la Nkasi Kasikazini Mh. Aida Khenan ambaye alisema kuwa huduma za afya kupitia bima hiyo hazina uhalisia wa kile kinachotarajiwa.

Dkt. Mollel alisema kuwa kinachoangaliwa ni mfumo wa bima ambapo kwa sasa fedha zinaenda ofisi ya mkuu wa mkoa na kisha kuna asilimia zinazokwenda vituo vya afya kupitia wilayani na kuwa hilo wameliona na watakwenda kutafuta ufumbuzi ili kasoro zitakazobainika ziondolewe.

Pia Dkt. Mollel aliitumia fursa hiyo kuwafunda watumishi wa afya kufanya kazi zao kwa weledi na kuwa wao kama wizara wamebaini mambo mengi ya hovyo yanayofanywa na watumishi hao na kuwa sasa wanachokifanya ni kukutana nao na kuelezana ili baadae watakapoanza kuchukua hatua kusiwepo na lawama.

Alisema kuwa changamoto ya dawa inayopatikana katika hospitali zetu ni matokeo ya utendaji hafifu kwa baadhi ya watendaji katika idara kwa kuwa serikali ilishatoa muongozo mzuri wa upatikanaji wa dawa na kuwa ukosefu wa dawa katika baadhi ya hospitali ni wizi na kutowajibika kwa watendaji hao.

‘’sisi kama wizara tumebaini madudu mengi yanayofanywa katika hospitali zetu na ndiyo maana tumekubaliana tupite kwanza kwa watumishi tuwafunde ili ukifika wakati tusilaumiane kutokana na maamuzi hayo magumu’’alisema

Awali mkuu wa wilaya ya Nkasi Mh. Said Mtanda alimweleza Naibu Waziri huyo kuwa ujenzi wa hospitali ya wilaya umekamilika kwa asilimia 97 huku Tshs,Bil.1.8 zimeshatumika kwenye ujenzi wa hospitali hiyo.

Alisema kuwa kilichobaki sasa ni kuiomba serikali iwapelekee mahitaji muhimu yanayotakiwa ili hospitali hiyo ifunguliwe rasmi na watu kuendelea kupata huduma za kiafya.

Ndipo naibu waziri alipomtaka mganga mkuu wa wilaya kuandika mahitaji muhimu yanayotakiwa kwenda MSD haraka ili hospitali hiyo iendelee kufanya kazi.

Mwisho

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa