• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Rukwa atoa wito ufuatiliaji wa karibu katika ugawaji wa vyandarua kwa Mkoa mzima

imewekwa Tar: August 9th, 2017

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Kamishna Mstaafu Zelote Stephen ametoa wito kwa watekelezaji wa mpango wa mpango wa taifa wa kudhibiti malaria katika Mkoa kufanya ufuatiliaji wa karibu ili kuepuka matatizo yaliyojitokeza katika mfumo uliotangulia.

Ametoa wito huo alipokuwa akifungua mkutano wa uhamasishaji kuhusu mpango wa ugawaji wa vyandarua kupitia vituo vya kutolea huduma za afya uliowashirikisha wakurugenzi wa Halmashauri, Wakuu wa Wilaya pamoja na waganga wakuu wa Halmashauri na Mkoa.

Ugawaji huu wa vyandarua ulikuwa ukijulikana kwa jina la Hati Punguzo uliokuwa ukitumia vocha maaluma na kulipia Shilingi 500, mpango ambao ulisitishwa mwaka 2014 kutokana na ubadhirifu uliotokea kwenye vituo vya kutolea huduma za afya ambapo watopa huduma walikuwa wakishirikiana na wakala kuandika vocha hewa na wakala kuchukua fedha bila ya kutoa huduma.

“kutokana na umuhimu wa kuwakinga wajawazito na watoto chini yam waka mmoja Serikali imeamua kuanzisha utaratibu wa ugawaji wa vyandarua kwa mjamzito na mtoto chini yam waka mmoja, moja kwa moja kutoka kwa mtoa huduma ya afya bila ya malipo yoyote wala uwakala,” Mh. Zelote alisema.

Aliongeza kuwa lengo la mpango huu ni kupunguza vifo vya wajawazito na watoto chini ya miaka mitano vinavyosababishwa na ugonjwa wa malaria. Pia kuongeza upatikanaji na utumiaji wa vyandarua katika ngazi ya kaya na jamii kwa asilimia 85 au zaidi na mwishoni mwa mwezi wa nane mwaka 2017 vyandarua hivyo vitaanza kugaiwa kwa mkoa wa Rukwa.

Kwa upande wake muuguzi mkuu mwandamizi kutoka wizara ya afya Bi. Epiphania Malingumu alisema kuwa mgawo wa vyandarua hivyo utafanyika kupitia bohari ya dawa (MSD) na vituo vya serikali pekee ndivyo vitaweza kutoa vyandarua hivyo kwakuwa vina namba maalum kwaajili ya malipo, hivyo vituo binafsi havitaweza kutoa huduma hii.

“Mama mjamzito atapata chandarua katika hudhurio la kwanza kliniki haijtajalisha ni mimba ya miezi mingapi, kama amehudhuria kliniki kwa mara ya kwanza akiwa na ujauzito wa miezi nane basi atapewa chandarua na mtoto akizaliwa atapewa tena chandarua na kama amejifungua mapacha basi atapewa vyandarua viwili,” Alisema.

Tafiti za mwaka 2015/2016 zinaonesha maambukizi ya ugonjwa wa malaria ni alimia 14.8 kitaifa na kwa Mkoa wa Rukwa ni asilimia 2.7. kwa mwaka 2012 maambukizi yalikuwa asilimia 9.5 kitaifa na kimkoa ilikuwa asilimia 4.5 ambayo imepungua kwa asilimia 1.8.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa