• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo aanza na watumishi ofisini kwake kuwataka kutojihusisha na siasa

imewekwa Tar: January 9th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaonya watumishi wa ofisi ya mkuu wa mkoa huo juu ya kutojihusisha na siasa hasa katika kipindi hiki cha kuelekea katika uchaguzi mkuu wa madiwani, wabunge na rais na kuwataka kutunza siri za serikali na kuachana na kawaida ya kupiga picha nyaraka za serikali na kuzisambaza katika mitandao ya kijamii hali inayokiuka maadili ya utumishi wa umma.

Amesema kuwa kuna tabia ya watumishi wa ofisi hiyo kujihusisha na kuwa mawakala wa wanasiasa na kutahadharisha kutotumia vibaya nafasi walizonazo na kwaajili hiyo wajiwekeze kwenye kuendeleza shughuli za kimaendeleo za mkoa kwani endapo nafasi hiyo itawatoka hawatakuwa na namna zaidi ya kuhangaika kutafuta ajira katika taasisi zisizo za kiserikali ambazo upatikanaji wake sio rahisi.

“Kipindi hiki ni cha pirika pirika nyingi za kisiasa na wengine wanapenda kufanya siasa tukumbuke kwamba sisi ni watumishi wa serikali hatupaswi kufanya siasa kazini lakini pia ni lazima tutunze siri za ofisini kwetu, tusitumike, watumishi wa Regional Secretariat wasijihusishe kuwa mawakala wa wanasiasa, imetokea mara kadhaa tunaona mtu anaipiga picha barua ya serikali halafu kwenye mtandao, watumishi tutunze siri za ofisi,” alisisitiza.

Aidha, amewataka watumishi hao kupunguza matumizi ya simu wakati wa kazi na kumuagiza Katibu Tawala wa Mkoa kuhakikisha huduma ya mtandao inayopatikana katika ofisi hiyo inatumika kwaajili ya shughuli za ofisi na kuongeza kuwa watumishi hao bado wanahitaji kufundishwa namna ya kuongea vizuri na wateja wanaofika kupata huduma katika ofisi hizo.

Halikadhalika, Mh. Wangabo amemtaka Katibu Tawala wa Mkoa kuhakikisha anaweka utaratibu maalum kwaajili ya kulipa maadeni yanayodaiwa na watumishi hao ili kuleta ufanisi wa kazi katika ofisi, na kuwataka watumishi hao kujitathmini katika uwajibikaji na uchapakazi, na kuwa na tabia ya kutunza vifaa vya ofisi ili kutumia fedha nyingine katika maendeleo.

Mh. Wangabo ameyasema hayo wakati alipofanya kikao na watumishi wa Sekretarieti ya Mkoa juu ya tathmini ya utendaji kazi kwa mwaka 2019 pamoja na kuwashukuru kwa ushirikiano wao katika wa kazi pamoja na uchache wao jambo ambalo serikali inalifanyia kazi ili kuongeza watumishi.  

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE( CSEE) 2025 January 31, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO SUMBAWANGA; ASISITIZA UMUHIMU WA HATI MILIKI ZA MAENEO YA TAASISI

    January 29, 2026
  • UKAGUZI WA MIRADI YA MAENDELEO; RC MAKONGORO AHIMIZA UBORA NA KUZINGATIWA KWA MUDA WA UTEKELEZAJI NKASI DC

    January 28, 2026
  • KUMBUKIZI YA KUZALIWA RAIS SAMIA; RC MAKONGORO AMUUNGA MKONO KWA KUONGOZA WANANCHI RUKWA KUPANDA MITI 4565

    January 27, 2026
  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa