• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC WANGABO ASISITIZA UMOJA KANISA LA KKKT RUKWA.

imewekwa Tar: December 25th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesisitiza umoja na mshikamano kwa waumini wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT)ambao kwa majuma kadhaa wamekuwa na mikwaruzano hali iliyofanya waumini hao kuswali kwa mafungu jambo ambalo halileti maendeleo ndani ya kanisa pamoja na mkoa.

Amesema kuwa wakati alipoteuliwa na Rais Dkt. John Pombe Magufuli na kuweza kuwasili katika mkoa miongoni mwa viongozi wa dini waliomuombea alikuwa ni Baba Askofu Ambele Mwaipopo ambaye anatambuliwa na serikali na kutahadharisha kuwa endapo serikali inamtambua kuwa ndio kiongozi wa kanisa hilo iweje wanaushirika wasimtambue.

“Mimi niko ndani ya Kanisa, nalitambua Kanisa, namtambua Muasham Baba Askofu, Kanisa hili limesajiliwa, Kanisa la Mungu, Muasham Baba Askofu wakati nilipofika tu hapa Mkoa wa Rukwa, Sumbawanga. Pamoja na viongozi wengine waliofika ofisini wakaniombea, Baba Askofu huyu alikuja akaniombea pia, wewe ni nani usiyemtambua? Mimi niwatake na kuwaomba, wanausharika wote ambao wako nje ya Kanisa warudi ndani ya Kanisa,” Alisema.

Na kuongeza kuwa endapo waumini wakishikana Mungu huwa pamoja na waumini hao na kamwe Mungu hawezi kumfuata mtu asiyependa umoja na kuwahahakikishia kuwa wale wote ambao wapo nje ya Kanisa kuwa Baba Askofu amekwisha wasamehe hivyo wasiwe na sababu ya kuendelea kubaki nje ya Kanisa.

Aidha alisisitiza kuwa umoja kati ya waumini wa madhehebu mbalimbali ndani ya mkoa unachangia kwa kiasi kikubwa umoja wa wanarukwa na hivyo kusababisha mkoa wa Rukwa kusonga mbele kimaendeleo.

Ameyasema hayo katika salamu zake za Krismasi leo 25.12.2019 kwa wananchi wa Mkoa wa Rukwa alizozitoa wakati aliposhiriki ibada ya ya Krismasi katika kanisa la KKKT Dayosisi ya Ziwa Tanganyika Mkoani Rukwa.

Kwa upande wake Baba Askofu Ambele Mwaipopo alimshukuru Mkuu wa Mkoa huyo kwa kutoa ujumbe mzuri wa mshikamano hasa katika siku ya kusheherekea kumbukumbu ya kuzaliwa Yesu Kristo na kuwaomba waumini waliohusdhuria ibada hiyo kuzungumza na wale wote waliopo nje ya kanisa hilo ili kuweza kuurudisha umoja na kuweza kupanga mambo ya kimaendeleo.

“Tukumbuke tuna mkakati mzuri kabisa wa kuandikwa wa dayosisi yetu ambayo tulikuwa tunayafanya, tumeweka kipaumbele lakini baada ya mgogoro huu kwakeli kulikuwa na kusimama mahala Fulani lakini Mungu ni mwema hajatuacha ndiomaana shughuli hizi hapa Kanisani zinaendelea na tunashukuru sana kwa kututia moyo Mkuu wa Mkoa kwaajili ya Ujenzi wa Kanisa hili,” Alisema

Aliongeza kuwa pamoja na kuwa Mkuu wa mkoa ni Muumini wa Kanisa la Roma lakini kwa upendo wake na kuguswa na jambo hilo ameona asali pamoja na washirika wa kanisa la KKKT.

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa