• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wanafunzi 10,250 wajiunga kidato cha kwanza huku ufaulu wa darasa la saba ukipanda Rukwa.

imewekwa Tar: December 15th, 2018

WANAFUNZI wapatao 15,193 sawa na asilimia 73, ambao wamefaulu mtihani wa kumaliza elimu ya msingi na 10,250 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza katika shule mbalimbali za sekondari mkoani Rukwa.

Ofisa elimu mkoa wa Rukwa, Nestory Mloka alisema hayo wakati wa kikao cha kutangaza matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu na uchaguzi wa wanafunzi wa kidato cha kwanza kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Rukwa.  


Mloka alisema kuwa kati ya wanafunzi hao 15,193 wavulana ni 7,545 na wasichana ni 7,648 kati ya watahiniwa 21,295 waliosajiliwa kufanya mtihani huo sawa na asilimia 82.19 ya walioandikishwa.

Alisema watahiniwa 482 sawa na asilimia 2.26 hawakuweza kufanya mtihani kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za utoro na magonjwa.

Alisema kwamba kutokana na ufaulu huo mkoa umepanda kwa asilimia 4.95 ambao ni 73 ukilinganisha na ufaulu wa mwaka 2017 ambao ulikuwa asilimia 68.05 huku Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi ikiongoza kwa wastani wa asilimia 83.40 ikifuatiwa Manispaa ya Sumbawanga, Kalambo na Sumbawanga vijijini ikiburuza mkia.


“Idadi ya wanafunzi wanaotakiwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2019 imeongezeka. Jumla ya wanafunzi 4,943 sawa na asilimia 32.53 hawajachaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kwa mwaka 2019 kutokana na upungufu wa vyumba vya madarasa na hivyo kusubiri chaguo la pili.” Alisema.


Naye, Kaimu Katibu tawala wa mkoa huo, Winnie Kijazi alisema licha ya ufaulu kuonyesha umepanda kwa asilimia nne, bado wadau wa elimu hawapaswi kujivunia kwa kuwa mkoa huo umeporomoka kutoka nafasi ya 15 mwaka 2017 hadi 18 mwaka 2018.


Kijazi alielekeza kuwa ni jukumu la kila Halmashauri kuweka mpango kazi na mpango mkakati wa kufikia asilimia lengwa kwa mujibu wa mwongozo wa matokeo makubwa sasa (BRN) na kuongeza kuwa miongoni mwa mikakati itakayowekwa ni pamoja na ufuatiliaji wa mara kwa mara wa ufundishaji na ujifunzaji shuleni na kudhibiti utoro wa wanafunzi katika shule.

Hata hivyo mkoa umeendelea kupandisha ufaulu mwaka hadi mwaka ambapo mwaka 2015 asilimia 55.25, mwaka 2016 asilimia 66, mwaka 2017 asilimia 68.05 na mwaka 2018 asilimia 73.

Matangazo

  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KIDATO CHA PILI 2025 November 05, 2025
  • RATIBA YA MTIHANI WA KUMALIZA ELIMU YA MSINGI 2025 August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa