• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo awaonya wanarukwa kutokuwa chanzo cha mauaji

imewekwa Tar: January 15th, 2020

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaonya wananchi wanaokaa karibu na milima ya Lyamba Lyamfipa kuacha maramoja kufanya shughuli za kibinaadamu katika milima hiyo baada ya shughuli hizo kuharibu mazingira na vyanzo vya maji vilivyomo na matokeo yake kuwasababishia maisha magumu wananchi wanaoishi katika bonde la ziwa Rukwa lililozungukwa na milima hiyo.

Amesema kuwa kuwa na maji ni jambo zuri lakini kuendelea kubaki nayo kwa miongo kadhaa ijayo ni jambo kubwa zaidi na kuongeza kuwa milima hiyo ndio chanzo cha maji cha Ziwa Rukwa, ziwa lililobeba jina la mkoa na hivyo kutokuwepo kwa ziwa hilo ni kuondoa asili ya mkoa jambo ambalo hataruhusu litokee.

“Milima hii yote ndio chanzo cha maji cha watu wanaoishi bonde la Ziwa Rukwa pamoja na Ziwa Rukwa lenyewe, mkiharibu hiyo milima hiyo ni sawa na kufanya mauaji kwa watu wanaoishi katika bonde la Ziwa Rukwa, kwasababu watakosa maji wale wananchi lakini hata mifugo itakosa maji huko lakini tatu hata ziwa rukwa lenyewe litakauka litajaa tope kwa hivyo vitendo vya kibinaadamu vya kukata miti na maji yaliyopo yatakwisha litafutika,” Alisisitiza

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipofanya ziara katika vijiji vilivyo karibu na milima ya Lyamba Lyamfipa katika Wilaya ya Nkasi na Sumbawanga na kuendelea kutoa elimu kwa wananchi hao juu ya utunzaji wa vyanzo vya maji na milima hiyo ili kupunguza athari za mvua zinazowatokea watu wanaoishi katika bonde la Ziwa Rukwa.

Amesema kuwa kutotunza vyanzo vya maji na vyanzo vya mvua kutasababisha kilimo chetu kutokuwa na tija na kueleza kuwa milima hiyo ndio tegemezo kwa mkoa wa Rukwa pamoja na mikoa ya jirani na hivyo utunzaji wake ni umuhimu kwa nchi.

Ameongeza kuwa mahala ambapo pamefyekwa na kulimwa si sawa na mahali ambapo hapajalimwa na penye miti kwani mvua ikija itachimba mahali ambapo pameshaharibika na kuacha maeneo ambayo yana miti na nyasi.

Katika hatua nyingine amewataka wananchi hao kuwa watulivu na kutoshawishiwa na wanasiasa wasiopenda utulivu uliopo hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi mkuu wa Madiwani, Wabunge na Rais.  

 

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa