• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

RC Wangabo Kupita Kijiji hadi Kijiji kuwasaka wajasiliamali wasio na vitambulisho.

imewekwa Tar: February 4th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka watendaji wa vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga kuhakikisha hadi kufikia mwishoni mwa mwezi wa pili wakamilishe zoezi la kuwatambua wajasiliamali waliopo kwenye maeneo yao, kuwasajili pamoja na kuwapa vitambulisho na kuahidi kupita Kijiji hadi Kijiji kuona kuwa zoezi hilo linafanikiwa kwa ukamilifu.

Mh. Wangabo amewaonya watendaji hao wa vijiji 112 kuwa mwananchi wa Kijiji chochote atakayebainika kuendelea kufanya biashara hali ya kuwa hana kitambulisho Mtendaji wa Kijiji hicho atakuwa maekwenda kinyume na maagizo na hivyo kuwa matatani na kuongeza kuwa wigo wa walipa kodi kwa mkoa wa Rukwa ni mdogo mno hivyo kulinganisha na mahitaji yaliyopo ndani ya mkoa na hivyo kuwataka wajasiliamali wote kuona umuhimu wa kuwa na kitambulisho hicho ili kutambulika na serikali kama mfanyabiashara mdogo.

“Pale mheshimiwa rais aliposema wafanyabiashara ndogondogo wasibughudhiwe alikuwa na maana kwamba ni lazima wawe na vitambulisho, kwamba wewe hustahili kulipa kodi ya TRA, sasa wewe hulipi kodi ya TRA nah una kitambulisho kinachokujulisha kwamba wewe ni mfanyabiashara mdogomdogo, sasa wewe uko wapi, uko ndani ya nchi hii ama wewe ni Mkongo au Mzambia, sasa baada yah apo itabidi usumbuliwe na tutakusumbua,” Alinaisha Mh. Wangabo.

Ameyasema hayo katika kikao kazi kilichowakutanisha watendaji wa Vijiji wa Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga katika Kijiji cha Mtowisa, Kata ya Mtowisa ili kuzungumzia mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitatu ya serikali ya awamu ya tano katika Halmashauri hiyo pamoja na kuwakumbusha majukumu yao kama wawakilishi wa serikali katika ngazi ya Kijiji.

Akielezea utaratibu wa kupata kitambulisho hicho Meneja wa Mamlaka ya Mapato Mkoa wa Rukwa Fredrick Kanyiriri alisema kuwa kabla ya kupewa kitambulisho ni lazima ujaze fomu ambazo zinapatikana kwa watendaji wa kata pamoja na watendaji wa vijiji na mitaa ndipo uweze kupatiwa kitambulisho hicho baada ya kulipia shilingi 20,000/= na kuongeza kuwa fomu hizo ni bure ila ukibainika kuwa umeidanganya serikali hatua za kisheria lazima zichukuliwe.

“Kikubwa ni kuhakikisha kuwa huyo mtu aidha ana TIN kwa maana ya kwamba analipa kodi ya TRA na kama hana TIN basi mtu huyo anatakiwa apatiwe kitambulisho, pia mnaweza kukutana na wengine waliotutoroka, mtu anaweza akakwambia kuwa mimi nalipa kodi ya mapato ni lazima akuthibitishie, atakuwa na ile TIN na risiti yake,” Alifafanua.

Akieleza makundi yanayostahili kupatiwa vitambulisho hivyo Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule amewata kuwa ni waendesha bodaboda, wauza mafuta petrol vijijini, wauza pombe za kienyeji, mama ntilie, wauza matunda, waziba pancha za baiskeli, wauza nyanya na mboga mboga, wachinjaji wa mifugo pamoja na wale wote wanaofanya biashara ambayo mapato ghafi hayajafikia shilingi milioni nne kwa mwaka.

Aliongeza kuwa kwenye fomu hizo za kujaza kabla ya kupewa kitambulisho kuna sehemu ya picha hivyo picha hiyo si muhimu kwani kitambulisho hicho kina namba tu na hakina picha hivyo mjasilimali kama atakuwa amesahau kitambulisho hicho anachotakiwa kufanya ni kukariri namba ya kitambulisho hicho pindi atakapoulizwa ili asibughudhiwe.

Waliosajiliwa kulipa kodi ya mapato katika Mamlaka ya Mapato (TRA) kwa Mkoa mzima wa Rukwa ni 18,199 kati hao walipa kodi 7,787 hawalipi na hivyo kubakiwa na walipa kodi 10,412 kati ya wananchi zaidi ya milioni 1.2 wa Mkoa wa Rukwa.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa