• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania PMO - Regional Administration and Local Government Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Industry, Trade and Investiment
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
      • KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
      • KITENGO CHA MAENDELEO YA JAMII
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Serikali ipo inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo, muhimu kudumisha amani – RC Wangabo

imewekwa Tar: April 5th, 2021

Mkuu wa mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewatoa wasiwasi wananchi Mkoani Rukwa ambao bado wamekuwa wakijiuliza maswali juu ya uelekeo wa serikali na nchi baada ya kifo cha aliyekuwa Rais wa Tanzania Hayati Dkt. John Pombe Magufuli kilichotokea tarehe 17.3.2021.

Mh. Wangabo amesema kuwa tangu nchi hii ipate uhuru mwaka 1961 ni miaka 60 imepita na sasa imepata rais wa Sita Mwanamke, tukio ambalo ni la kihistoria na kuongeza kuwa kinamama kwa miaka mingi wamekuwa shupavu katika kuongoza familia hasa malezi ya Watoto na hivyo kuwaomba wananchi wote kuziongoza familia zao kumuunga mkono Rais Samia Suluhu Hassan ilia pate nguvu na Afya na kuleta maendeleo katika nchi yetu.

“Najua kila mmoja wetu sasa hivi anatafakari kwa kina kwamba nchi sasa hivi tunaelekea wapi, niwahakikishie kwamba serikali ipo, inafanya kazi vizuri na itaendelea kuwepo na sisi tupo, tunachotaka sisi ni amani ili nchi iweze kusonga mbele, lakini kikubwa Zaidi niwaombe tuendelee kumuombea Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia, tumuombee san ana tuwaombee viongozi wote wa serikali ili serikali yetu isiyumbe iwe thabiti na kwa maongozi ya Mwenyezi mungu tutafika.”

“Sina shaka, Rais wetu anatutosha, lakini anahitaji kuungwa mkono, mshikamano na amani na utulivu kutoka kwetu, bila ya shaka wanarukwa wote, tunalifanya hili na tumeanza kulifanya na tutaendelea kulifanya la kuleta amani, na tumeshuhudia tuna amani ya kutosha, tuendelee nayo, lakini tusione mtu ana ngeu ama amevunjika mguu kesho ama keshokutwa, mtaleta dosari,” Alisisitiza.

Mh. Wangabo ameyasema hayo alipokuwa akitoa salamu zake za Pasaka katika Kanisa Katoliki Parokia ya Kristo Mfalme Mjini Sumbawanga baada ya Ibada ya Pasaka ambapo wakristo wote nchini wanaungana na wenzao duniani kusheherekea sikukuu hiyo.

Aidha, katika kuhakikisha Watoto yatima hawaachwi nyuma Mh. Wangabo alipitisha ‘Bakuli’ kwa waumini waliohudhuria ibada hiyo ili kupata fedha za kununua baadhi ya mahitaji kwaajili ya Watoto yatima wa kituo cha Mtakatifu Maria Goreth kilichopo Katandala mjini Sumbawanga, ambapo katika mchango huo ilipatikana Shilingi 188,600/= na kuzikabidhi kwa Padri Canute Mwageni Paroko wa Parokia ya Kristo Mfalme Mjini Sumbawanga

Matangazo

  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA KIDATO CHA PILI 2025 January 10, 2026
  • MATOKEO YA MTIHANI WA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE 2025 January 10, 2026
  • UCHAGUZI WA WANAFUNZI WA KIDATO CHA KWANZA, 2026 December 06, 2025
  • RATIBA YA UPIMAJI WA KITAIFA WA DARASA LA NNE August 20, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • WATUMISHI WA AFYA RUKWA WAHIMIZWA KUTOA ELIMU KWA WANANCHI KUHUSU BIMA YA AFYA KWA WOTE

    December 17, 2025
  • BODI YA USHAURI YA HOSPITALI YA RUFAA SUMBAWANGA YAZINDULIWA, YAAGIZWA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA MENEJIMENTI KUBORESHA HUDUMA.

    November 28, 2025
  • PPRA YAANZA MAFUNZO KUWEZESHA MAKUNDI MAALUM KUSHIRIKI UNUNUZI WA UMMA

    December 25, 2025
  • RC MAKONGORO AONGOZA KIKAO CHA KAMATI YA AMANI RUKWA , ASISITIZA UOMJA NA KULINDA AMANI KWA MAENDELEO YA MKOA

    November 20, 2025
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa