• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wananchi watakiwa kujitokeza kupeleka watoto wenye miezi 9 hadi 59 kupata chanjo.

imewekwa Tar: October 16th, 2019

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewataka wananchi Mkoani Rukwa kuhakikisha wanajitokeza kwa wingi kupeleka watoto wenye umri kuanzia miezi 9 hadi 59 kupata chanjo katika kampeni ya kitaifa ya utoaji wa chanjo ya Surua Rubella iliyoanza kufanyika kuanzia tarehe 17 hadi 21 Oktoba, 2019.

Chanjo hiyo ya kuzuia magonjwa ya Surua na Rubella ilizinduliwa na kuanza kutolewa rasmi nchini Tanzania mwezi Aprili, 2014 na kuanzia kipindi hicho imeanza kutolewa hadi sasa. Kampeni hiyo itakwenda sambamba na utoaji wa chanjo ya Polio ya Sindano (IPV) kwaajili ya kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa kupooza.

“Jumla ya watoto 163,564 wenye umri wa kati ya miezi 9 hadi miezi 59 wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya Surua Rubella na jumla ya watoto 92,879 wenye umri kati ya miezi 18 hadi 42 wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya polio ya sindani katika mkoa wa Rukwa kupitia kampeni hii,” Alisema.

Aidha alisema kuwa ni jukumu la kila mwananchi kutimiza wajibu wake katika kufikisha ujumbe kwa wananchi ili watoto wote walio katika makundi yaliyotajwa wapatiwe huduma hii muhimu kwaajili ya taifa la kesho lenye afya njema na kuwataka wananchi kujiepusha na Imani na mila zinazoweza kudhoofisha zoezi hili muhimu na kuwatoa hofu kuwa chanjo hizo ni salama na hazina madhara.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Dkt. Boniface Kasululu amesema kuwa kwa lengo la kupunguza msongamano na kuhakikisha watoto wote wanapata huduma hii muhimu, wakati wa Kampeni huduma za chanjo zitatolewa katika maeneo ya vituo vya kutolea huduma za afya na kwa baadhi ya maenee yenye changamoto ya umbali, watoa huduma kutoka kwenye vituo vya kutolea huduma watakwenda kutoa huduma ngazi ya jamii.

“Lengo la chanjo hii ni kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa Surua Rubella, ugonjwa ambao ulikuwa ukiongoza kwa kusababisha vifo vya watoto wengi wenye umri chini ya miaka 5 nchini Tanzania na Mkoa wa Rukwa kwa ujumla, kwa kawaida chanjo hii hutolewa dozi mbili; dozi ya kwanza inatolewa kwa mtoto anapofikisha umri wa miezi 9 na dozi ya pili akifikisha umri wa miezi 18 na kamapeni hii ni kwa watoto wote bila ya kujali walikwishapata au hawajapata chanjo hii,” alisisitiza.

Kauli mbiu ya Kampeni hii ni “ Chanjo ni Kinga kwa Pamoja Tuwakinge.”

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa