• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Watendaji wanaochangia kuenea kipindupindu Rukwa kushughulikiwa

imewekwa Tar: May 23rd, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesema hatamvumilia mtendaji wa serikali atakaechangia kuenea kwa ugonjwa kipindupindu katika mkoa kwani elimu ya ugonjwa huo imeshatolewa kwa muda mrefu hivyo ni jukumu la kila mtendaji kuhakikisha ugonjwa huo unatokomezwa.

Amesema kuwa kumekuwa na tabia iliyojengeka ya watendaji kuanza kufanya majukumu yao baada ya mlipuko wa ugonjwa huo kutokea na kuonya kuwa kaya ambayo haitakuwa na choo katika ngazi ya Kijiji basi mtendaji wa Kijiji atawajibishwa.

“Wakati hatua mbalimbali zikiendelea kuchukuliwa, tukikidhibiti kipindupindu halafu kikatokea tena hapo mahali ambapo kimetokea hatutapaelewa, watendaji wetu wakitilia maanani  wakahakikisha kaya zetu zina vyoo na kuchemsha maji hatuwezi kuwa na kipindupindu, sasa kinatokea kipindupindu halafu kaya haina choo, mtendaji wa Kijiji hicho hana sababu ya kuwa mtendaji,” Alisisitiza.

Ameyasema hayo alipokuwa akifunga kikao cha dharura kilichoitishwa na kamati ya afya ya mkoa ili kujadiliana juu ya mbinu za kutokomeza ugonjwa huo ambao umeathiri zaidi ya watu 600 tangu kulipukwa kwake mwezi November mwaka 2017 na kutoweka mwezi Machi mwaka 2018 na hatimae kuibuka tena tarehe 6, Mei mwaka 2018.

Kikao hicho kilichojumuisha, Wakuu wa ilaya, Wakurugenzi wa halmashauri, Wenyeviti wa halmashauri, madiwani, kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa na wilaya, Maafisa Afya wa mkoa na halmashauri, wataalamu wa afya pamoja na waganga wakuu wa wilaya na mganga mkuu wa mkoa kiliazimia kutokomeza ugonjwa huo na kuweka mikakati ya kutorejea tena wa ugonjwa huo.

Akisoma baadhi ya maazimio Katibu Tawala wa Mkoa Benard makali amesema kuwa kamati ya afya za vijiji na vitongoji zisimamiwe kutenda majukumu yake kwani wao ndio wanaojuana zaidi katika utekelezaji wa maagizo na sheria za serikali kuanzia ngazi hizo na kuitaka kamati za afya za Wilaya kuwa na mbinu za kudumu za kuthibiti ugonjwa huo na kutaka elimu zaidi iendelee kutolewa.

Tangu kulipuka tena kwa ugonjwa huo tarehe 6, Mei mwaka 2018 wagonjwa 9 wamefariki na wengine 214 wakiendelea kupatiwa matibabu katika vituo mbalimbali vya Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga ambayo imeathirika zaidi huku wananchi wake wakiwa na asilimia 36 ya umiliki wa vyoo bora.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa