• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Watu 17 wafariki kwa kichaa cha Mbwa Mkoani Rukwa.

imewekwa Tar: September 28th, 2018

Watu 17 wamefariki Mkoani Rukwa katika kipindi cha mwaka 2017/2018 kutokana na ugonjwa wa kichaa cha mbwa unaosababishwa na virusi vinavyojulikana kwa jina la “Lyssavirus” ambapo hushambulia mfumo wa fahamu na kusababisha kifo kwa binadamu na mnyama.

Hayo yamejulikana katika maadhimisho ya siku ya kuhamasisha udhibiti wa ugonjwa wa kichaa cha Mbwa duniani yaliyofanyika Kimkoa katika viwanja vya Nelson Mandela Manispaa ya Sumbawanga mwishoni mwa mwezi wa tisa, mwaka 2018.

Akisoma taarifa fupi ya ugonjwa huo mtaalamu wa magonjwa ya wanyama wa Mkoa Dkt. Respich Maengo amefafanua kuwa ugonjwa huo pia husambazwa na paka ambapo mtu aking’atwa au kukwaruzwa na paka mwenye kichaa pia husababisha binadamu kuupata ugonjwa huo.

“Mbwa waliopata chanjo dhidi ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa Mkoani Rukwa ni asilimia 14.6 ambao ni mbwa wachache sana na kati ya paka 9,514 waliopo, hakuna hata paka mmoja aliyepata chanjo hiyo, hii inaonyesha wazi kuwa wananchi hawaijali mifugo yao,” Alisema.

Maengo alieleza dalili za ugonjwa huo kwa binadamu kuwa mwanzoni hazieleweki vizuri kwani huanza kwa maumivu ya kichwa, homa na kuchoka kwa mwili na hatimae unavyoendelea mgonjwa huanza kukosa usingizi, kuwa na hasira na kuchanganyikiwa, kutokwa na mate mengi, kushindwa kumeza chakula, kuogopa kuangalia maji na kasha kufariki.

Shirika la Afya Duniani (WHO) linashauri kuchanja si chini ya ailimia 70 ya mbwa wote, na katika Mkoa wa Rukwa mbwa waliochanjwa mwaka 2017/2018 ni 6,017 sawa na asilimia 14.6, huku Manispaa ya Sumbawanga ikiwa imechanja 30.5%, Halmashauri ya Wilaya ya Sumbawanga 15.3%, Halmashauri ya Wilaya ya Kalambo 6.3%, Halmashauri ya Wilaya ya Nkasi 7.3%.

Mwaka 2017/2018 watu walioumwa na mbwa ni 1,050 na vifo ni 17. Maadhimisho ya mwaka huu yanaendeshwa na kauli mbiu “Ugonjwa wa kichaa cha mbwa: Sambaza ujumbe okoa Maisha.”

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa