• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wenyeviti wa vijiji wapewa onyo kali kuhusu vitambulisho vya NIDA

imewekwa Tar: April 18th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaonya vikali wenyeviti wa vijiji wananojihusisha na kuwajazia watu wasio raia wa Tanzania fomu za mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA) ili kuhalalisha uwepo wao katika nchi na kuongeza kuwa kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria.

Pia aliwaasa wananchi kuwa macho na wale wanaopewa fomu hizo hali ya kuwa sio raia na hawastahili kupewa vitambulisho hivyo na kuwasisitiza kuwa walinzi wa kwanza wa taifa la Tanzania ili wananchi ambao ni raia wa Tanzania wanaostahili kupata fomu hizo ndio wapatiwe.

“Mwenyekiti yoyote wa Kijiji akibainika amemwandikisha mtu amabae sio raia, ambae hastahili na hana vibali husika vinavyomruhusu apate kitambulisho cha taifa, ukibainika tunakukamata tunakuweka ndani, halafu tunakufungulia mashataka kwasababu utakuwa msaliti na unalisaliti taifa letu, na nyie wananchi ndio macho yetu yeyote mnaeona sio raia na amepewa fomu muwekeeni kipingamizi, kwasababu sheria inaruhu,” Alisema.

Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha mtowisa, kata ya mtowisa, wilayani Sumbawanga alipokwenda kutemebelea na kuijionea miradi kadhaa ya kimaendeleo inayoendelea kutolewa katika ukanda  wa bonde la ziwa Rukwa.

Kwa upande wake Mratibu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya taifa (NIDA)Mkoani Rukwa Emanuel Mjuni amesema kuwa katika kata ya Mtowisa wanatarajia kuwaandikisha wananchi 5,430 na kusisistiza kuwa wale wasiokuwa wakazi wa kata hiyo hawana vigezo vya kupata fomu na hatimae kukosa vigezo vya kupata vitambulisho hivyo vya taifa.

“Kama tukiwaandikisha wananchi ambao hawaishi kwenye maeneo yetu wale wananchi ambaotumewaandalia fomu hizo watakosa, kama Mh. Mkuu wa Mkoa alivyosema wale wenyeviti na watendaji wa vijiji wasimamie kwa makini kuhakikisha yule anaepata fomu ni mkazi halali wa eneo husika na zoezi hili linafanyika nchi nzima hivyo basi wale ambao wapo huku kibiashara ama kwa mambo mengine warudi kwenye maeneo yao ili waandikishwe, ili wasikose vitambulisho,” Alisisitiza.

Majibu hayo yaliibuka baada ya maswali kadhaa kutoka kwa wananchi Pius Wapinda na Paulo Chipeta waliotaka kujua endapo ni ruhusa kwa wafanyabiashara kuchukua fomu za maombi ya vitambulisho vya taifa katika eneo ambalo zoezi hilo limemkuta ili aweze kuchukua fomu na kupata kitambulisho na hatimae kuwa na utambulisho wa uraia wa nchi yake na pia hatua zitakazochukuliwa kwa wenyeviti watakaokiuka taratibu za kutoa fomu.

Matangazo

  • RATIBA YA MTIHANI WA KIDATO CHA SITA 2025 April 15, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA PILI 2024 January 04, 2025
  • MATOKEO YA KIDATO CHA NNE 2024 January 23, 2025
  • MATOKEO YA DARASA LA NNE 2024 January 04, 2025
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • RC MAKONGORO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO, ARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA UMEME

    May 05, 2025
  • JAMII YAASWA KUJENGA UTAMADUNI WA KUWAHUDUMIA WAZEE

    March 19, 2025
  • KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA TAMISEMI YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI MKOA WA RUKWA

    January 09, 2025
  • RAIS SAMIA ATOA ZAWADI ZA MSIMU WA SIKUKUU WA MWAKA MPYA KWA WATOTO YATIMA NA WENYE MAHITAJI MAALUM MKOANI RUKWA

    December 31, 2024
  • Angalia Zote

Video

LIVE- WAZIRI MCHENGERWA ANATAO TANGAZO LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Mfumo wa Kutuma, Kupokea na kufuatilia Malalamiko, Mapendekezo, Maulizo na Pongezi
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa