• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • MMM |
    • Baruapepe za watumishi |
Rukwa Region
Rukwa Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Rukwa

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati ya Mkoa
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti
    • Idara
      • Utawala na Rasilimali watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Afya na Ustawi wa Jamii
      • Menejimenti ya Serikali za Mitaa
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Ukaguzi wa Ndani
      • TEHAMA
      • Huduma za Kisheria
      • Fedha na Uhasibu
      • Ugavi
  • Wilaya
    • Wilaya ya Sumbawanga
    • Wilaya ya Nkasi
    • Wilaya ya Kalambo
  • Halmashauri
    • Manispaa ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Sumbawanga
    • H/Wilaya ya Nkasi
    • H/Wilaya ya Kalambo
  • Fursa za Uwekezaji
    • Viwanda
    • Utalii
    • Madini
    • Kilimo
    • Ufugaji
    • Uvuvi
    • Miundombinu ya Rukwa
  • Huduma zetu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za Afya
    • Huduma ya Elimu
    • Huduma za Kilimo
    • Livestocks
    • Huduma za Uvuvi
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Ripoti
    • Huduma za Kisheria
    • Fomu Mbalimbali
    • Fedha
    • Mpango Mkakati
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Videos
    • Hotuba
    • Picha
    • Habari
    • Matukio
    • Waliofaulu na Waliochaguliwa Shule

Wenyeviti wa vijiji wapewa onyo kali kuhusu vitambulisho vya NIDA

imewekwa Tar: April 18th, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amewaonya vikali wenyeviti wa vijiji wananojihusisha na kuwajazia watu wasio raia wa Tanzania fomu za mamlaka ya vitambulisho vya taifa (NIDA) ili kuhalalisha uwepo wao katika nchi na kuongeza kuwa kufanya hivyo ni ukiukwaji wa sheria.

Pia aliwaasa wananchi kuwa macho na wale wanaopewa fomu hizo hali ya kuwa sio raia na hawastahili kupewa vitambulisho hivyo na kuwasisitiza kuwa walinzi wa kwanza wa taifa la Tanzania ili wananchi ambao ni raia wa Tanzania wanaostahili kupata fomu hizo ndio wapatiwe.

“Mwenyekiti yoyote wa Kijiji akibainika amemwandikisha mtu amabae sio raia, ambae hastahili na hana vibali husika vinavyomruhusu apate kitambulisho cha taifa, ukibainika tunakukamata tunakuweka ndani, halafu tunakufungulia mashataka kwasababu utakuwa msaliti na unalisaliti taifa letu, na nyie wananchi ndio macho yetu yeyote mnaeona sio raia na amepewa fomu muwekeeni kipingamizi, kwasababu sheria inaruhu,” Alisema.

Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kijiji cha mtowisa, kata ya mtowisa, wilayani Sumbawanga alipokwenda kutemebelea na kuijionea miradi kadhaa ya kimaendeleo inayoendelea kutolewa katika ukanda  wa bonde la ziwa Rukwa.

Kwa upande wake Mratibu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya taifa (NIDA)Mkoani Rukwa Emanuel Mjuni amesema kuwa katika kata ya Mtowisa wanatarajia kuwaandikisha wananchi 5,430 na kusisistiza kuwa wale wasiokuwa wakazi wa kata hiyo hawana vigezo vya kupata fomu na hatimae kukosa vigezo vya kupata vitambulisho hivyo vya taifa.

“Kama tukiwaandikisha wananchi ambao hawaishi kwenye maeneo yetu wale wananchi ambaotumewaandalia fomu hizo watakosa, kama Mh. Mkuu wa Mkoa alivyosema wale wenyeviti na watendaji wa vijiji wasimamie kwa makini kuhakikisha yule anaepata fomu ni mkazi halali wa eneo husika na zoezi hili linafanyika nchi nzima hivyo basi wale ambao wapo huku kibiashara ama kwa mambo mengine warudi kwenye maeneo yao ili waandikishwe, ili wasikose vitambulisho,” Alisisitiza.

Majibu hayo yaliibuka baada ya maswali kadhaa kutoka kwa wananchi Pius Wapinda na Paulo Chipeta waliotaka kujua endapo ni ruhusa kwa wafanyabiashara kuchukua fomu za maombi ya vitambulisho vya taifa katika eneo ambalo zoezi hilo limemkuta ili aweze kuchukua fomu na kupata kitambulisho na hatimae kuwa na utambulisho wa uraia wa nchi yake na pia hatua zitakazochukuliwa kwa wenyeviti watakaokiuka taratibu za kutoa fomu.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI October 24, 2023
  • TAARIFA KWA UMMA - MAPOKEZI YA FEDHA KIASI CHA SHILINGI BILIONI 3.8 KWA AJILI YA SEKTA YA AFYA October 05, 2023
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI- RUKWA September 27, 2023
  • MATOKEO YA KIDATO CHA SITA 2023 July 13, 2023
  • Angalia Zote

Habari Mpya

  • UMOJA NA MSHIKAMANO SILAHA ZA MAFANIKIO MIAKA 62 YA UHURU

    December 09, 2023
  • MAKONGORO AWATAKA WADAU KUILIPA TEMESA KWA WAKATI

    November 21, 2023
  • MAPAMBANO DHIDI YA MALARIA; WANAFUNZI RUKWA KUGAWIWA VYANDARUA

    October 19, 2023
  • MAKONGORO ATAKA MIRADI IKAMILIKE KABLA YA OKTOBA 30, 2023.

    October 18, 2023
  • Angalia Zote

Video

Serikali Kuimarisha mahusiano na Sekta Binafsi
Video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Miundombinu ya Rukwa
  • Uvuvi
  • Mikakati ya Mkoa
  • Industries
  • Madini
  • Speeches
  • Huduma za Kilimo
  • Regional History
  • Hotuba

Viunganishi Linganifu

  • Pakua Salaryslip yako hapa
  • Idara ya Takwimu (NBS)
  • Kilio cha Wananchi kinasikilizwa
  • Watumishi portal
  • Tafuta ajira Serikalini
  • Pata kila kitu kutoka serikalini

World visitors tracker

world map hits counter

Wapitiaji

free HitCounter

Ramani Elekezi

Wasiliana nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, 1 Barabara ya Mkoani

    Sanduku la barua: Box 128 Sumbawanga, 55180 RUKWA

    Simu: 025 280 2137

    Simu: 0735019734

    barua pepe: ras@rukwa.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa