Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amefanikisha kupatikana kwa ekari 3 ili kujengwa kwa nyumba za askari polisi katika eneo la karibu na kituo cha polisi kipya kinachomaliziwa kujengwa katika kata ya Mtowisa, Wilayani Sumbawanga na kurahisisha makazi ya polisi katika bonde la ziwa Rukwa.
Hayo yamejiri ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya wananchi wa kata ya Mtowisa kwa Mkuu wa Mkoa waliyoiahidi tarehe 13.11.2017 Mh. Wanagabo alipofanya ziara katika eneo hilo na kudai kuwa usalama wa bonde hilo sio mzuri kwa kukosa kituo bora cha polisi na makazi yao na kupelekea kuanzisha ujenzi wa kituo na hatimae kuomba nguvu ya Mkuu wa Mkoa kuweza kumalizia ujenzi huo.
Kaimu Meneja wa Wakala wa Misitu Wilaya ya Kalambo aelezea maajabu yanayopatikana katika maporomoko ya Kalambo.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amepiga marufuku mwalo wa mwambao wa Kijiji cha Kirando kutumika kama bandari baada ya kufika katika mwalo huo na kukuta lori likiwa linapakua mizigo kwa lengo la kusafisirisha mizigo kwenda kwenye visiwa vya ziwa Tanganyika. Amesema kuwa wananchi wasipotoshe malengo ya mwalo huo ambayo ni kwaajili ya kuuza na kununua samaki wavuliwao kwenye ziwa Tanganyika, “Lengo la Mwalo huu ni kuuzia samaki na dagaa lakini naona mizigo hii, imegeuzwa kuwa bandari, narudia aliyoyasema Mh. Mbunge (Ali Kessy) irudishwe kwenye hali yake ile ile,” Alisisitiza
Hakimiliki © 2017 Mkoa wa Rukwa. Haki Zote Zimehifadhiwa